HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, April 15, 2019

RC MAKONDA AWAONYA TBA, ATAKA PESA ZILIZOTOLEWA NA RAIS MAGUFULI KUTUMIKA KUKAMILISHA MIRADI KWA WAKATI

*Aeleza kutofurahishwa na kasi na utekelezaji wa miradi katika Manispaa ya Ilala

Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda leo Aprili 13 amefanya ziara ya ukaguzi wa miradi mbalimbali inayotekelezwa katika  Wilaya ya Kigamboni na kuwaagiza Wakala wa Majengo ya serikali nchini (TBA) kuhakikisha wanakamilisha kwa haraka ujenzi wa majengo ya Halmashauri ya wilaya ya Kigamboni, Ofisi ya Mkuu wa wilaya pamoja  na nyumba za viongozi kabla ya Juni 30 mwaka huu.

 Makonda amesema kuwa wakala hiyo ikishindwa kutekeleza agizo hilo watachukuliwa hatua ikiwemo kunyang'anywa mradi, kurudisha fedha na vifaa viliyobaki vilevile watalazimika kulipa kodi ya jengo la mtu binafsi linalotumiwa kama Ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyi.

Hayo yamekuja baada ya  wa  Mkuu wa Mkoa kuchukizwa na hali ya kusuasua katika utekelezaji wa miradi hiyo licha ya kuongezewa muda zaidi ya mara mbili na fedha zote za ujenzi walishapatiwa lakini utekelezaji umekuwa duni hali inayopelekea  serikali kuzidi kutumia mamilioni ya pesa kulipa kodi ya pango kwenye jengo la mtu binafsi linalotumika kama ofisi ya mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wa Kigamboni.

Akiwa katika mradi wa ujenzi wa jengo la hospitali ya Wilaya ya Kigamboni  Makonda ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa mradi huo uliogharimu takribani bilioni 1.5 kutoka Serikalini na amemuagiza mkandarasi kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha jengo linakabidhiwa kabla ya Juni 30 mwaka huu.

Kwa upande wake Mratibu mkuu wa Wakala wa Majengo ya serikali (TBA) Mkoa wa Dar es salaam Mhandisi Wilson Tesha amemuahidi RC Makonda kuwa wakala hiyo itahakikisha wanakamilisha ujenzi kabla ya Juni 30 kama walivyoagizwa.

Vilevile Mkuu wa Mkoa huyo ameitaka halmashauri ya Manispaa ya Ilala kujitathimini kuhusiana na miradi inayotekelezwa kwa kuwa hafurahishwi na utendaji kazi wao ambapo amesema kuwa shilingi bilioni 14 za ujenzi wa mtaro katika mto Msimbazi zimetengwa ila hakuna kinachoendelea na amemwagiza Mkurugenzi kuita kikao cha madiwani mapema jumanne ili wampe maelezo ya kina kuhusu kinachokwamisha utendaji kazi katika miradi husika.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad