HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, March 8, 2019

WANAWAKE TPA WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUTOA MSAADA MUHIMBILI

 Mmoja wa wafanyakazi wa TPA, Zahara Malika akikabidhi moja kati ya katoni za Biscuit na misaada mbalimbali walizozitoa katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili kitengo cha Moi kwa wazazi wenye watoto wenye Kichwa kikubwa na mgongo wazi ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani ambayo kilele chake ni leo. Wengine pichani ni baadhi ya wanawake kutoka TPA waliowatembelea watoto hao hospitalini hapo leo na anayepokea kwa niaba ya wagonjwa wengine ni Nesi wa hospital hiyo, Bi Rehema Ally. 
 Mmoja wa wafanyakazi wa TPA, Hilda Mwakatobe akikabidhi moja kati ya katoni za juisi na misaada mbalimbali walizozitoa katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili kitengo cha Moi kwa wazazi wenye watoto wenye Kichwa kikubwa na mgongo wazi ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani ambayo kilele chake ni leo. Wengine pichani ni baadhi ya wanawake kutoka TPA waliowatembelea watoto hao hospitalini hapo leo na anayepokea kwa niaba ya wagonjwa wengine ni Bi. Cheusi Selemani.
Baadhi ya wanawake ambao ni wafanyakazi wa TPA wakiwasili katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili kitengo cha Moi kwa wazazi wenye watoto wenye Kichwa kikubwa na mgongo wazi ili kuwatembelea na kuwapa misaada ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani ambayo kilele chake ni leo.
 Mkurugenzi wa Fedha wa TPA, Bi. Nuru Mhando akimbeba mmoja wa watoto wenye kichwa kikubwa na mgongo wazi waliolazwa katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili kitengo cha Moi ambacho wamelazwa watoto hao ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani ambayo kilele chake ni leo.
Baadhi ya wanawake ambao ni wafanyakazi wa TPA wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukabidhi misaada mbalimbali na pesa taslimu kwa wazazi wenye watoto wenye Kichwa kikubwa na mgongo waliolazwa katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili kitengo cha Moi. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad