HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, March 8, 2019

Airtel Divas washerehekea siku yao kwakushukuru wanaume wote

Airtel DIVAS Ikiwa ni siku ya wanawake inayoadhimishwa ulimwenguni kote wanawake wote wanaofanya kazi katika vitengo mbalimbali ndani ya kampuni ya simu za mkononi ya Airtel (Airtel Divas)  leo wamesherehekea kwa style ya kipekee ambapo wamewashukuru wanaume wote wanaofanya nao kazi kila siku kwa kuwapatia zawadi.

Akiongoza wanawake wenzie wote (Airtel Divas) katika maadhimisho hayo Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali watu Stella Kibacha alisema “leo ni siku yetu Wanawake, ambapo inaadhimishwa dunia nzima kila tarehe 3 Machi. Lakini style yetu sisi Divas  wa Airtel tumeamua kuwashuru kwa zawadi  mwanaume wote hapa Airtel, ni ukweli kuwa tunashinda nao kila siku wanatuonyesha ushirikiano wa kutosha, hawana ubaguzi tunafanya kazi kwa usawa na kusikilizana, kwa kweli tunawashukuru sana”

Kibacha alieleza kuwa “Mwaka huu kauli mbiu ya siku ya wanawake ni ‘#BalanceforBetter’ ikipambanua mambo mengi kati yao ni kujipanga na kupangilia kila jambo ili kuwa na mafanikio”

“Airte Divas Tumejipanga kisawasawa kuhakikisha kila jambo kazini au nyumbani yanakaa sawa kwa manufaa yetu na taifa kwa ujumla” alializa kwa kusema Kibacha
 Airtel Divas Mkurugenzi wa Airtel Rasilimali watu Stella Kibacha akimshukuru mmoja kati ya wafanyakazi wa airtel wakiume bw Dunia Yusufu leo walipoadhimisha siku ya wanawake Duniani yenye kauli mbiu ‘Balance for better’. Siku ya wanawake huadhimishwa kila mwaka tarehe 08 machi ikiwa na lengo la kutambua mchango wa wanawake katika jamii.
 Airtel Divas Meneja uhusiano Airtel Dangio Kaniki akitoa zawadi kwa Edward Mtingwa kwa lengo la kuwashukuru wanaume wote wanaofanya kazi nao. ‘Airtel Divas’ leo wameadhimisha siku ya wanawake Duniani yenye kauli mbiu ‘Balance for better’ kwa kutoa shukrani kw wanaume wote. Siku ya wanawake huadhimishwa kila mwaka tarehe 08 Machi ikiwa na lengo la kutambua mchango wa wanawake katika jamii
 Airtel Divas Mkurugenzi wa Airtel Huduma kwa wateja Adriana Lyamba akitoa zawadi kwa Ezekieli Mwakangata ikiwa ni ishara ya kushukuru wanaume wote wanaofanya kazi na wafanyakazi wa Airtel ‘Airtel Divas’ leo walipoadhimisha siku ya wanawake Duniani yenye kauli mbiu ‘Balance for better’ kwa kutoa shukrani kwa wanaume wote. Siku ya wanawake huadhimishwa kila mwaka tarehe 08 Machi ikiwa na lengo la kutambua mchango wa wanawake katika jamii. 
Airtel Divas wakiwa kwenye picha ya pamoja leo wakati wa  maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani yaliyobeba kauli mbiu ‘Balance for better’ Siku ya wanawake huadhimishwa kila mwaka tarehe 08 Machi kwa lengo la kutambua mchango wa wanawake katika jamii


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad