HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, March 11, 2019

NMB yazindua ‘Floti Fasta’ kwa Mawakala wao

VINARA wa huduma za kibenki nchini, Benki ya NMB, wamezindua huduma ya kidijitali ya kuwawezesha Mawakala wa NMB kupata mkopo wa salio la kuhudumia wateja ‘Floti Fasta,’ kupitia NMB Mobile na NMB KLiK pindi wanapoishiwa salio.

Floti Fasta ni huduma ya uwezeshaji, inayolenga kuwapa nguvu ya ziada mawakala wa NMB waliotapakaa kila kona, kupata salio la dharura wanalohitaji kuhudumu nyakati za usiku ama wikiendi, wanapokosa huduma za kuongeza salio katika matawi ya benki hiyo.

Huduma hiyo ya kwanza na ya aina yake nchini, imezinduliwa mwishoni mwa wiki, ikilenga kukuza mitaji ya mawakala, lakini pia kuwasaidia kukuza biashara zao, huku wakitengeneza ajira kwa Watanzania wengi kupitia biashara zao za NMB Wakala.

Kiwango cha chini cha kupata salio kupitia ‘Floti Fasta’ni Sh. 50,000 na kiwango cha juu ni Sh. Milioni 5, huduma ambayo haina riba, bali mwombaji atatozwa asilimia 3 itakayojumuisha Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT), ambako tozo litafanyika kabla ya mkopo kutolewa.

Akizungumza wakati wa kuzindua Floti Fasta, Mkuu wa Kitengo cha Malipo na Akaunti, Michael Mungure, aliscma kuwa huduma hiyo, itawawezesha zaidi ya mawakala 6,800 kukuza biashara zao na kuwapa uwezo wa kuhudumia wateja wao muda wote.

“Kupilia huduma hii ya Floti Fasta, tatizo la kuishiwa salio kwa mawakala wetu limepatiwa ufumbuzi, Mteja anatakiwa kutumia NMB Mobile au NMB KliK kuweza kupopa hususani kwa nyakati ambazo hakuna huduma za kibenki kama usiku ama wikiendi,” alisema Mungure.

Mungure aliongeza kuwa: “Dhamira yetu kila siku imekuwa ni kubuni bidhaa na huduma bora kwa kuangalia changamoto mbalimbali za kifedha nchini na kuzipatia suluhu.

“Imekuwa wazi kuwa kuna changamoto kubwa kwa mawakala ya kuishiwa floti na hivyo kusababisha wateja kutopata huduma stahiki za kutoa na kuweka fedha hususani baada ya matawi ya NMB kufungwa.

“Tulipoliona hili tukaona ni fursa kubwa kutoa suruhisho la kifedha ambalo ni rafiki kwa mawakala kupitia NMB Mobile na NMB KLiK,” alisisitiza Mungure.

Mawakala wa NMB wana mchango mkubwa katika utoaji wa huduma za kifedha na hivyo kuchangia ukuaji wa uchumi wa Taifa, ambapo Mungure amebainisha kuwa NMB ikiwa kama benki kubwa hapa nchini, inaona umuhimu wa kuwasaidia mawakala wake ilikukidhi mahitaji ya soko.

“Kwa sasa, wateja wanaopata huduma za kifedha kupitia NMB Wakala wana uhakika wa kupata huduma pasipo hofu ya kukosa floti, kwani kupitia huduma hii, Mawakala wa NMB wanakuwa ndio wa uhakika zaidi katika utoaji huduma za kifedha muda wowote na sehemu yoyote,” alisema.

Mungure alisema kuwa, pamoja na kwamba huduma hiyo imeanzishwa kwa ajili ya kuwasaidia mawakala wa NMB, faida yake inakwenda mbali zaidi na kumfikia hata asiye mteja wa NMB, ambaye ataweza kulipa Kodi za Serikali na bili kama za Dawasco, LUKU, muda wa maongezi na kulipa ving’amuzi.

 Mkuu wa Kitengo cha Biashara Benki ya NMB, Donatus Richard akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu huduma mpya ya kiditali Floti Fasta. Katikati ni  Mkuu wa malipo na akaunti, Michael Mungure na kulia ni Mkuu wa Kitengo cha wakala, Ericky Willy.

Mkuu wa Kitengo cha Biashara Benki ya NMB, Donatus Richard akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu huduma mpya ya kiditali Floti Fasta. Kulia ni Mkuu wa malipo na akaunti, Michael Mungure.
 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad