HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, January 9, 2019

TANROADS MKOANI PWANI KUTUMIA BIL. 25.4 MATENGENEZO YA BARABARA

Na Mwamvua Mwinyi
WAKALA wa Barabara Tanzania (TANROADS) mkoani Pwani ,unatarajia kutumia kiasi cha sh.bilioni 25.4 kwa ajili ya kufanya matengenezo mbalimbali ya barabara kwa bajeti ya mwaka 2018-2019. Hayo yalisemwa mjini Kibaha na meneja wa TANROADS mkoani hapo, mhandisi Yudas Msangi,  wakati wa kikao cha bodi ya barabara cha mkoa huo .

Alieleza, hadi kufikia septemba 2018 zimepokelewa kiasi cha sh. milioni 958.7  kwa ajili ya matengenezo mbalimbali. "Katika kipindi hicho kiasi cha shilingi bilioni mbili zimetumika kufanya matengenezo mbalimbali kwenye barabara kuu", 

"Kazi za matengenezo zilichelewa kuanza kutokana na taratibu za manunuzi na uhakiki wa mikataba ambavyo huchukua muda mrefu kukamilika hasa mikataba inayohakikiwa kwa mwanasheria mkuu wa serikali"alisema Msangi. Aidha Msangi alibainisha, mkoa umepanga kufanya miradi ya maendeleo ya barabara zenye urefu wa kilometa 32.5 zenye thamani ya sh.bilioni 2.3.

Alisema,meneja huyo alisema kwenye miradi hiyo ya maendeleo sh. bilioni 1.3 ni bajeti ambapo sh.milioni 969 ni kutoka mfuko wa barabara vilevile bilioni 7.5 ni kutoka serikali zitafanya ukarabati kwa kiwango cha changarawe/udongo. Nae mkuu wa  mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo alieleza, ili kuboresha barabara za mkoa huo watendaji wanapaswa kuwa waadilifu.

"Kutokana na mkoa kuwa na viwanda vingi uboreshaji wa miundombinu ya barabara utasaidia kuinua uchumi wa wananchi na Taifa":" Pia Muwe makini na baadhi ya watu wanaoharibu miundombinu ya barabara ," alisema Ndikilo.
 Mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo akizungumza jambo wakati wa kikao cha bodi ya barabara mkoani hapo akizungumza jambo. (Picha na Mwamvua Mwinyi) 
Baadhi ya wajumbe wa kikao cha bodi ya barabara mkoani Pwani wakisikiliza jambo. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad