Kaimu
Mkurugenzi mkazi wa USAID Tanzania David Thompson (wa tatu kushoto)
akimkabidhi mfano wa funguo wa gari Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala
za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo(katikati) wakati
wa hafla fupi ya kukabidhi magari mawili kwa Wizara hiyo leo Jijini Dar
Es Salaam. Wa kwanza kulia ni Dk. Marina Njelekela, Wa Tatu kulia ni
Mkurugenzi wa Deloitte Consulting LTD, Carlton Jones na wapili kulia
ni Naibu Katibu Mkuu-TAMISEMI Dkt Zainabu Chaula.
Na Mathew Kwembe
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani
Jafo amepokea magari mawili yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni
200 na kusema kuwa magari hayo yataongeza thamani katika juhudi za
serikali za kuimarisha utoaji wa huduma bora za afya katika mikoa ya
Lindi na Mtwara.
Akiongea
katika hafla ya makabidhiano hayo, Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa USAID
Tanzania David Thompson aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa dhamira
yake ya kuboresha viwango vya afya kwa watanzania wote.
“Kupitia
msaada huu, Serikali ya Marekani inaungana na Serikali ya Tanzania
kurahisisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa watu wote, katika
jamii za watu wa Lindi na Mtwara, mkazo zaidi ukiwa kwa wanawake na
vijana,” alisema.
Kabla
ya kuyapokea magari hayo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika
la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID) David Thompson, Waziri
Jafo alisema kuwa anatambua kazi nzuri inayofanywa na Serikali ya
Marekani kupitia Mradi wa USAID Boresha Afya kanda ya kusini.
Alisema
kuwa kwa kutambua kazi nzuri inayofanywa na mradi wa Boresha Afya
katika mikoa ya Morogoro, Iringa, Njombe, Lindi, Mtwara na Ruvuma anayo
furaha kubwa kushiriki katika hafla hiyo ya kupokea magari hayo yenye
thamani ya Tsh.219, 372,136.
“Kwa
niaba ya Serikali ya Tanzania ningependa kuwafikishia shukrani zetu za
dhat kwa Serikali ya Marekani na wote walio katika mradi huu wa USAID
Boresha Afya Kanda ya kusini,” alisema.
Waziri Jafo aliongeza kuwa serikali inajivunia kushirikiana na washirika ambao kweli wanajali hali za raia wa Tanzania.
Alisema
kuwa kupitia msaada huo USAID Boresha Afya Kanda ya kusini imeonyesha
kweli iko pamoja na watanzania katika kusimamia changamoto za afya
nchini.
Waziri
Jafo alitoa wito kwa Wakuu wa Mikoa ya Lindi na Mtwara kuhakikisha kuwa
magari hayo yanatunzwa kwani hiyo itawatia moyo washirika wa maendeleo
kuendelea kutoa misaada zaidi.
Aidha
Waziri Jafo alisema Serikali katika kuboresha huduma za afya nchini
katika kipindi cha miezi 12 iliyopita imefanikiwa kukamilisha vituo vya
afya 210 na hivyo inasubiri kupatiwa madawa kutoka bohari kuu ya madawa
nchini.
Aliongeza
kuwa katika kipindi cha miezi 18 ijayo Serikali inatarajia kukamilisha
ujenzi wa vituo vya afya 340 ambapo vituo 100 vitaweza kutoa huduma ya
upasuaji.
Kwa
upande wake Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali
za Mitaa anayeshughulikia Afya Dkt.Zainab Chaula aliishukuru Serikali
ya Marekani kwa msaada huo wa magari na kuongeza kuwa msaada huo
utajazia juhudi za serikali katika kuboresha huduma za Afya nchini.
Alisema
kuwa magari hayo yatatumiwa na Timu ya Usimamizi wa Afya katika Mikoa
ya Lindi na Mtwara katika kusaidia na kuimarisha usimamizi wa shughuli
zinazohusiana na VVU, uzazi wa mpango, Kifua Kikuu, Malaria, lishe,
jinsia, Jamii na nyinginezo zinazohusiana na afya.
Kwa
upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mtwara DKT Wedson Sichalwe na Mganga
Mkuu wa Mkoa wa Lindi DKt Genchwele Makenge waliishukuru serikali ya
Marekani kwa msaada huo kwani unakwenda sambamba na malengo ya serikali
ya kuboresha huduma za afya kwa jamii.
Mradi
wa USAID Boresha Afya Kanda ya Kusini ni mradi wa miaka mitano ulioanza
oktoba 2016 na unatarajia kukamilisha shughuli zake ifikapo mwezi
septemba mwaka 2021 unaotekelezwa na halmashauri 43 kwenye mikoa ya
Iringa, Njombe, Morogoro, Lindi, Mtwara na Ruvuma kwa kushirikiana na
mashirika ya kitaalamu ya FHI na EngenderHealth na Management and
Development for Health (MDH)
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Selemani Jafo akizungumza wakati wa kupokea msaada wa magari mawili
katika wizara hiyo yatakayotumika katika mikoa ya Lindi na Mtwara
kupitia mradi wa USAIDS Boresha Afya Kanda ya Kusini.
Kaimu
Mkurugenzi mkazi wa USAID Tanzania David Thompson akizungumza kuhusu
wanavosimamia miradi mbalimbali ya USAID hapa nchini Tanzania wakati wa
hafla fupi ya kukabidhi magari mawili kwa Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
Mkurugenzi
wa Deloitte Consulting LTD, Carlton Jones akizungumza kuhusu
wanavyosimamia mradi wa USAID Boresha Afya kanda ya Kusini unaotekelezwa
katika halmashauri 43 kwenye mikoa ya Iringa, Njombe, Morogoro, Lindi,
Mtwara na Ruvuma wakati wa kutoa msaada wa magari mawili kwa Ofisi ya
Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Selemani Jafo akiwasha moja ya gari mara baada ya kukabidhiwa magari
hayo mawili yatakayotumika kwenye kuimarisha usimamizi wa Shuguli
zinazohusiana na masuala ya Afya katika mikoa ya Lindi na Mtwara kupitia
mradi wa USAID Boresha Afya Kanda ya Kusini.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Selemani Jafo(kulia) akimkabidhi mfano wa funguo ya gari Mganga Mkuu wa
Mkoa wa Mtwara, Dk. Wedson Sichalwe(kushoto) ili kusaidia na kuimarisha
usimamizi wa Shughuli zinazohusianana na VVU, Uzazi wa mpango. Katikati
ni Kaimu Mkurugenzi mkazi wa USAID Tanzania David Thompson
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Selemani Jafo(kulia) akimkabidhi mfano wa funguo ya gari Mganga Mkuu wa
Mkoa wa Lindi, Dk. Genchwele Makenge(kushoto) ili kusaidia na
kuimarisha usimamizi wa Shughuli zinazohusianana na VVU, Uzazi wa
mpango. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi mkazi wa USAID Tanzania David
Thompson
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Selemani Jafo akiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kukabidhiwa
magari mawili na USAID kupitia mradi wa USAID Boresha Afya kanda ya
Kusini unaotekelezwa katika halmashauri 43 katika mikoa ya Iringa,
Njombe, Morogoro, Lindi, Mtwara na Ruvuma.
Baadhi
ya wageni waalikwa wakiwa kwenye hafla fupi ya kukabidhi magari mawili
kwa Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI).
Magari yaliyotolewa na USAID kupitia mradi wa USAID Boresha Afya kanda ya Kusini yatakayosaidia masuala ya Afya katika mikoa ya Lindi na Mtwara.
No comments:
Post a Comment