Kaimu
 Mkurugenzi mkazi wa USAID Tanzania David Thompson (wa tatu kushoto) 
akimkabidhi mfano wa funguo wa gari Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala
 za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo(katikati) wakati
 wa hafla fupi ya kukabidhi magari mawili kwa Wizara hiyo leo Jijini Dar
 Es Salaam. Wa kwanza kulia ni Dk. Marina Njelekela, Wa Tatu kulia ni 
Mkurugenzi wa Deloitte Consulting LTD, Carlton Jones na wapili kulia 
ni Naibu Katibu Mkuu-TAMISEMI Dkt Zainabu Chaula.
Na Mathew Kwembe
Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani
 Jafo amepokea magari mawili yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 
200 na kusema kuwa magari hayo yataongeza thamani katika juhudi za 
serikali za kuimarisha utoaji wa huduma bora za afya katika mikoa ya 
Lindi na Mtwara.
Akiongea
 katika hafla ya makabidhiano hayo, Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa USAID 
Tanzania David Thompson aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa dhamira 
yake ya kuboresha viwango vya afya kwa watanzania wote.
“Kupitia
 msaada huu, Serikali ya Marekani inaungana na Serikali ya Tanzania 
kurahisisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa watu wote, katika 
jamii za watu wa Lindi na Mtwara, mkazo zaidi ukiwa kwa wanawake na 
vijana,” alisema.
Kabla
 ya kuyapokea magari hayo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika 
la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID) David Thompson, Waziri 
Jafo alisema kuwa anatambua kazi nzuri inayofanywa na Serikali ya 
Marekani kupitia Mradi wa USAID Boresha Afya kanda ya kusini.
Alisema
 kuwa kwa kutambua kazi nzuri inayofanywa na mradi wa Boresha Afya 
katika mikoa ya Morogoro, Iringa, Njombe, Lindi, Mtwara na Ruvuma anayo 
furaha kubwa kushiriki katika hafla hiyo ya kupokea magari hayo yenye 
thamani ya Tsh.219, 372,136.
“Kwa
 niaba ya Serikali ya Tanzania ningependa kuwafikishia shukrani zetu za 
dhat kwa Serikali ya Marekani na wote walio katika mradi huu wa USAID 
Boresha Afya Kanda ya kusini,” alisema.
Waziri Jafo aliongeza kuwa serikali inajivunia kushirikiana na washirika ambao kweli wanajali hali za raia wa Tanzania.
Alisema
 kuwa kupitia msaada huo USAID Boresha Afya Kanda ya kusini imeonyesha 
kweli iko pamoja na watanzania katika kusimamia changamoto za afya 
nchini.
Waziri
 Jafo alitoa wito kwa Wakuu wa Mikoa ya Lindi na Mtwara kuhakikisha kuwa
 magari hayo yanatunzwa kwani hiyo itawatia moyo washirika wa maendeleo 
kuendelea kutoa misaada zaidi.
Aidha
 Waziri Jafo alisema Serikali katika kuboresha huduma za afya nchini 
katika kipindi cha miezi 12 iliyopita imefanikiwa kukamilisha vituo vya 
afya 210 na hivyo inasubiri kupatiwa madawa kutoka bohari kuu ya madawa 
nchini.
Aliongeza
 kuwa katika kipindi cha miezi 18 ijayo Serikali inatarajia kukamilisha 
ujenzi wa vituo vya afya 340 ambapo vituo 100 vitaweza kutoa huduma ya 
upasuaji.
Kwa
 upande wake Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali
 za Mitaa anayeshughulikia Afya Dkt.Zainab Chaula aliishukuru Serikali 
ya Marekani kwa msaada huo wa magari na kuongeza kuwa msaada huo 
utajazia juhudi za serikali katika kuboresha huduma za Afya nchini.
Alisema
 kuwa magari hayo yatatumiwa na Timu ya Usimamizi wa Afya katika Mikoa 
ya Lindi na Mtwara katika kusaidia na kuimarisha usimamizi wa shughuli 
zinazohusiana na VVU, uzazi wa mpango, Kifua Kikuu, Malaria, lishe, 
jinsia, Jamii na nyinginezo zinazohusiana na afya.
Kwa
 upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mtwara DKT Wedson Sichalwe na Mganga
 Mkuu wa Mkoa wa Lindi DKt Genchwele Makenge waliishukuru serikali ya 
Marekani kwa msaada huo kwani unakwenda sambamba na malengo ya serikali 
ya kuboresha huduma za afya kwa jamii.
Mradi
 wa USAID Boresha Afya Kanda ya Kusini ni mradi wa miaka mitano ulioanza
 oktoba 2016 na unatarajia kukamilisha shughuli zake ifikapo mwezi 
septemba mwaka 2021 unaotekelezwa na halmashauri 43 kwenye mikoa ya 
Iringa, Njombe, Morogoro, Lindi, Mtwara na Ruvuma kwa kushirikiana na 
mashirika ya kitaalamu ya FHI na EngenderHealth na Management and 
Development for Health (MDH)
 Waziri
 wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 
Selemani Jafo akizungumza wakati wa kupokea msaada wa magari mawili 
katika wizara hiyo yatakayotumika katika mikoa ya Lindi na Mtwara 
kupitia mradi wa USAIDS Boresha Afya Kanda ya Kusini.
 Kaimu
 Mkurugenzi mkazi wa USAID Tanzania David Thompson akizungumza kuhusu 
wanavosimamia miradi mbalimbali ya USAID hapa nchini Tanzania wakati wa 
hafla fupi ya kukabidhi magari mawili kwa Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais 
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
Mkurugenzi
 wa Deloitte Consulting LTD, Carlton Jones akizungumza kuhusu 
wanavyosimamia mradi wa USAID Boresha Afya kanda ya Kusini unaotekelezwa
 katika halmashauri 43 kwenye mikoa ya Iringa, Njombe, Morogoro, Lindi, 
Mtwara na Ruvuma wakati wa kutoa msaada wa magari mawili kwa Ofisi ya 
Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
 Waziri
 wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 
Selemani Jafo akiwasha moja ya gari mara baada ya kukabidhiwa magari 
hayo mawili yatakayotumika  kwenye kuimarisha usimamizi wa Shuguli 
zinazohusiana na masuala ya Afya katika mikoa ya Lindi na Mtwara kupitia
 mradi wa USAID Boresha Afya Kanda ya Kusini.
Waziri
 wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 
Selemani Jafo(kulia) akimkabidhi mfano wa funguo ya gari  Mganga Mkuu wa
 Mkoa wa Mtwara, Dk. Wedson Sichalwe(kushoto) ili kusaidia na kuimarisha
 usimamizi wa Shughuli zinazohusianana na VVU, Uzazi wa mpango. Katikati
 ni Kaimu Mkurugenzi mkazi wa USAID Tanzania David Thompson 
 Waziri
 wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 
Selemani Jafo(kulia) akimkabidhi mfano wa funguo ya gari  Mganga Mkuu wa
 Mkoa wa Lindi, Dk. Genchwele Makenge(kushoto) ili kusaidia na 
kuimarisha usimamizi wa Shughuli zinazohusianana na VVU, Uzazi wa 
mpango. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi mkazi wa USAID Tanzania David 
Thompson 
 Waziri
 wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 
Selemani Jafo akiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kukabidhiwa 
magari mawili na USAID kupitia mradi wa USAID Boresha Afya kanda ya 
Kusini unaotekelezwa katika halmashauri 43 katika mikoa ya Iringa, 
Njombe, Morogoro, Lindi, Mtwara na Ruvuma.
Baadhi
 ya wageni waalikwa wakiwa kwenye hafla fupi ya kukabidhi magari mawili 
kwa Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa 
(TAMISEMI).
  Magari yaliyotolewa na USAID kupitia mradi wa USAID Boresha Afya kanda ya Kusini  yatakayosaidia masuala ya Afya katika mikoa ya Lindi na Mtwara.

No comments:
Post a Comment