Na Ripota Wetu,Globu ya jamii
MTOTO anayetambulika kwa jina la Thomas Rwembiza Renatus(9) anayesoma darasa la pili Shule ya Msingi Kilungule jijini Dar es Salaam amepotea na hajarudi nyumbani tangu juzi.
Imeelezwa kuwa mtoto huyo anaishi Kimara Bonyokwa mtaa wa Mavurunza na kwamba amepotea Septemba 26 alivyotoka asubuhi saa nne kuelekea shule.
Tayari familia ya mtoto huyo imetoa ripoti Polisi na kupewa RB.
Baba wa mtoto huyo amesema kwa atakayemuona atoe taarifa kituo chochote cha Polisi au awasiliane naye kwa namba ya simu 0652066366
No comments:
Post a Comment