HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, September 11, 2018

HABIBU KYOMBO AREJEA NCHINI BAADA YA KUMALIZA MAJARIBIO AFRIKA KUSINI

Na Agness Francis,globu ya jamii
UONGOZI wa Singida United  wanategemea kukaa mezani na Mamelod  Sundowns  ya Afrika Kusini kwa ajili ya kufikia muafaka wa mchezaji Habibu Kyombo.

Mshambuliaji huyo kinara kwa ufungaji kwenye michuano ya Azam Sport Federation Cup aliekipiga  Singida United kwa msimu mzima uliopita 2017-18 amerejea nchini jana akitokea nchini humo.

Ambako alikuwa akifanya majaribio katika viwanja vya Schloorkop Mamelodi Sundowns kwa ajili ya majaribio kikosini hapo.

Imeelezwa Kyombo alipewa siku 10 za majaribio na uongozi wa klabu ya Mamelod na  kuongezewa tena siku zingine 10 kwa ajili ya kufanya trial na senior team.

Siku 20 zilipokamilika kwa majaribio ya mshambuliaji huyo huku mamelodi wakikikubali kiwango chake na uwezo wake mkubwa aliouonyesha kwa siku hizo alizopewa.

Baada ya kukaa mezani uwongozi wa Singada United na Mamelod Sundown kujadiliana kubaki  mchezaji huyo kwa waajiri wake  wa msimu uliopita au kujiunga na kikosi cha Mamelodi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad