HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, September 28, 2018

BREAKING NEWS: WAANDISHI WAGOMEWA KUCHUKUA MATUKIO KATIKA UZINDUZI WA FILAMU YA WEMA SEPETU

Na Khadija Seif, Globu ya Jamii

Waandishi wa habari jioni hii wagomewa kuingia ndani Kwenye hafla ya uzinduzi wa filamu ya D.A.D ya Msanii wa kibongo nchini  wema sepetu maarufu kamaambayo amemshirikisha msanii kutoka nchi ya Ghana Van Vicker.

Akizungumza nje ya ukumbi Meneja wa Wema Sepetu, Martin Kadinda amesema shughuli hiyo ilishanunuliwa na moja ya chombo cha habari hapa nchini ambao wana mamlaka yote ya kurusha kwa matangazo ya moja kwa moja na kupiga Picha zote.

Mmoja wa wanahabari akiongea na Michuzi TV ameeleza kuwa ni vibaya kwani mpaka kuweza kuingia ndani ni lazima kulipa Dola elfu 20 .

Hivyo basi kitendo hiko kilichofanywa na waandaji wa shughuli hiyo kimewanyima nafasi wanahabari ,na sio la haki kwani mpaka alipofikia nguvu nyingi zimetokana na kushirikiana na wanahabari.

Kitendo hiko kinaweza kuibua matabaka,pamoja na chuki kutokana na ubaguzi huo uliofanyika katika hafla hiyo na watu kutafsiri vibaya kuwa imeonekana chombo hicho kuwa bora kuliko vingine.

Van Vicker aliwasii nchini jana kwa ajili ya uzinduzi wa filamu hiyo iliyofanywa miaka mitatu iliyopita.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad