HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, September 17, 2018

Bilioni 3.7 serikali zaliwa na Tanzania Remix

Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii
Tanzania Remix watapeli bilioni 3.7 fedha za serikali ambazo zilikuwa kwaajili ya fidia kwa wahanga wa upanuzi wa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Fedha hizo zilkuwa kwaajili ya kununua maeneo ya wananchi waliokuwa wananishi kipunguni A na Kipunguni Mashariki.

Akizungumza na wanachi wa kata ya Luhangwa Kata ya Msongola manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaamleo, Naibu waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Mhandisi Atashasta Nditiye alipotembelea viwanja vya fidia vya Luhangwa amesema kuwa serikali inataka viwanja ambavyo havina mgogoro na vilivyolipiwa kwa kuwa serikali ishalipia fedha viwanja vyote 537 ambavyo vinadhamani ya shilingi bilioni 3.7.

" Tanzania Remix ninawapa wiki moja kupima na kuwalipwa wananchi fedha zao za viwanja kulingana na mkataba wao. Msipofanya hivyo Jumatatu ya Septemba 24,2018 hamtaru nyumbani mtaenda sehemu tofauti na nyumbani " Amesema Nditiye.

"Tanzania Remix imelipwa Fesha ya viwanja 537 ambavyo  vinatakiwa kuwapa  wananchi wa kipungunj A na Kipunguni Mashariki kama ya fidia kwaajili ya upanuzi wa uwanja wa ndege na kwakuwa hawajawalipa wenyevinjwa leo tuhairishe shughuli ya ukaguzi wa viwanja na tuwape muda Tanzania Remix kuwalipa wenye viwanja kwa kadili ya walivyosaini mkataba".

Nditiye ameiagiza Tanzania Remix ifikapo Septemba 24 mwaka huu iwalipe fedha wananchi atakagua viwanja visivyo na mgogoro na wananchi vilivyopangiliwa vizuri kila kiwanja kikijitegemea na vyenye barabara zinazoeleweka.

Wananchi wa Luhangwa  wanena.
Mwenyekiti wa mtaa wa  Luhangwa, Salum Kipendo amesema kuwa yeye pamoja na anaowaongoza hatujalipwa fedha za viwanja kadiri ya mkataba unavyosema kwa asilimia 40 kwa Asilimia 60.

Nae Mrisho Hasimu miliki wa shamba amesema kuwa mimi na baadhi ya wenzangu hatujalipwa fedha za ununuzi wa viwanja kadili ya mkataba tuliosaini sisi na serikali kwaajili ya viwanja vya wananchi waliopisha  upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere.
 Mkurugenzi wa Mamlaka ya Viwanja wa ndege (TAA) Richard Mayongela akizungumza na wanachi wa Luhangwa Kata ya  Msongola jijjnj Dar es Salaam na kuwaambia kuwa wao mamlaka ya viwanja vya ndege wameshalipa fedha zote kwaajili ya viwanja waliobakia ni Tanzania Remix ambao wanatakiwa kuwalipa fedha hizo.
 Naibu waziri wa uchukuzi Mhandisi Atashazita Nditiye akizungumza na wananchi wa Luhanga kata ya Msongola Manispaa ya Ilala jijni Dar es Salaam alipotembelea viwanja vya fidia za wananchi  waliopisha upanuzi wa uwanja wa ndege na kuwapa  Tanzania Remix wiki moja kwaajili ya kuwalipa wananchi stahiki zao kwani serikali imeshatoa fedha kwaajili ya ununuzi wa viwanja hivyo.
  aibu waziri wa uchukuzi Mhandisi Atashazita Nditiye akitembelea viwanja vya fidia kwa wananchi waliopisha upanuaji wa uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mmilikiwa shamba eneo la Luhangwa,Seif Mbonde  akizungumza na Naibu waziri wa uchukuzi Atashazita Nditiye wakati alipotembelea eneo la viwanja vya fidia za wananchi walipisha upanuzi wa uwanja wa ndege wa malimu Julius Nyerere Luhanga kata ya Msongola manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam. 
Mmiliki wa shamba katika eneo la Luhangwa Mrisho Hashim akizungumza na waandishi wa habari katika eneo Luhangwa kata ya Msongola jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na kutolipwa sitahiki yake kadili ya Mkataba wao kati ya Tanzania Remix na baadhu ya wananchi wenye mashamba eneo la Luhangwa kata ya Msingola  Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam ikiwa bado hawajalipwa fedha za viwanja vyao kadili ya mkataba unavyosema.  



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad