HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, July 4, 2018

WERRASON APATA MWALIKO, KUTUA DAR KESHO

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MWANAMUZIKI nguli kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Werrason Ngiama Makanda, anatarajia kuwasili nchini kesho kwa ajili ya kufanya maonyesho tofauti katika mikoa ya Mwanza, Arusha na Dar es Salaam.

Mratibu wa ziara ya mwanamuziki huyo, Lengos VIP alisema kuwa mwanamuziki huyo nguli anawasili kesho saa 4 asabuhi kwa ajili ya maonesho hayo maalum yatakayofanyika sehemu tofauti nchini.

Alisema kuwa Mwanamuziki huyo ataanza onyesho la kwanza mkoani Arusha siku ya Ijumaa ya Julai 6 na siku ya pili ya Julai 7, atakuwa mkoani Mwanza huku onyesho la mwisho litafanyika Mkoani Dar es Salaam.

Alisema mkoani Arusha Mwamuziki huyo atafanya onyesho kwenye ukumbi wa Mjengoni Club, wakati Mwanza atafanya mambo yake kwenye ukumbi wa Rock City na Mkoa wa Dar es Salaam Life Park uliopo Mwenge (zamani Word Cinema).
                                                                        
Werrason aliyeanzia katika bendi ya Wenge BCBG,  miongoni mwa wanamuziki wa Congo wanaopata nafasi za kupata mwaliko wa kuja kutoa burudani hapa nchini,  huku mratibu wa maonyesho hayo akiwataka mashabiki wajitokeze kupata burudani nzuri kutoka kwa nguli huyo.

Mwanamuziki huyo amekuwa akifanya ziara katika nchi mbali mbali ikiwemo Tanzania na kufanya vizuri kwa mashabiki kukubali ujio wake.                                                                            

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad