HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, July 4, 2018

WAFANYABISAHARA KUTOKA NCHI SABA WATEMBELEA BANDARI YA DAR ES SALAAM

WAFANYABIASHARA kutoka nchi saba zinazotumia Bandari ya Dar es Salaam wameipongeza Serikali kwa kuondoa changamoto walizokuwa wakilalamikia hivyo kuahidi kuendelea kupitia mizigo yao bandarini hapo.

Hayo yamezungumzwa leo jijini Dar es Salaam wakati wafanyabiashara hao walipotembelea Bandari hiyo kujionea namna shuguli mbalimbali zinavyoendeshwa ambapo walisema hatua ya serikali kuondoa vikwazo imewapa moyo wa kurudi kupitiasha vizigo bandarini hapo.

Rais wa Wafanyabiashara wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Sumaili Edouard, alisema wamejipanga kurudi kwa kishindo kwa sababu dosari ambazo zilikuwa zimewakimbiza tayari zimeondolewa.

“Tunaipongeza serikali ya Tanzania kupitia Mamlaka ya Bandari (TPA) kwa kufanya juhudi kubwa ya kutuunganisha wafanyabiashara kutoka sehemu mbalimbali ili kwa pamoja kuendeleze biashara hapa nchini.

‘Vikwazo vyote ambavyo tulikuwa tunavilalamikia kama mizani, kodi nakadhalika, sasa hivi vimeondolewa hivyo tumerudi kwa kishindo ili kuleta changamoto kwa sababu tumeona Tanzania imeamka kwa kiasi kikubwa,’ alisema Edouard.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko akizungumza na wafanyabiashara kutoka nchi za Rwanda, Uganda, Burundi, Congo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Zambia, Malawi na Comoro kuhusu ufanisi wa bandari hiyo pamoja na mikakati waliyoiweka ili kuhudumia nchi nyingi waliotembelea bandari ya Dar es Salaam leo.
Kaimu Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Freddy Liundi akizungumza na wafanyabiashara kutoka nchi za Rwanda, Uganda, Burundi, Congo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Zambia, Malawi na Comoro kwenye kituo cha kuhifadhi mizigo ya nchini Uganda leo kwenye bandari ya jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Masomo Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini (TPA), Lydia Mallya akizungumza kuhusu TPA wanavyoshirikiana na nchi hizo ili mizogo yao inayoshushwa kupitia bandari hiyo inakuwa salama.
Afisa Mkuu wa Uendeshaji  kutoka TICTS Charlie Darazi akitoa ufafanuzi jinsi kampuni ya TICTS wanavyojishughulisha na kazi ya kushusha na kupakia mizigo katika bandari ya jijini Dar es Salaam wakati wa ziara ya wafanyabiashara kutoka nchi za Rwanda, Uganda, Burundi, Congo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Zambia, Malawi na Comoro.
 Wafanyabiashara kutoka nchi za Rwanda, Uganda, Burundi, Congo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Zambia, Malawi na Comoro wakitembelea bandari kujionea ufanisi wa wandari ya Dar es Salaam leo.
 Kaimu Mkurugenzi Masomo Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini (TPA), Lydia Mallya akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa ziara ya  Wafanyabiashara kutoka nchi za Rwanda, Uganda, Burundi, Congo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Zambia, Malawi na Comoro waliotembelea bandari hiyo leo jijini Dar es Salaam.
Rais wa Wafanyabiashara wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Sumaili Edouard akizungumza na waandishi wa habari kuhusu wafanaya biashara na nchi hiyo walivyoona ufanisi wa bandari ya Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad