Na Ripota Wetu, Arusha
MAMLAKA ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), imeanza kutekeleza mkakati wa kushirikishana na wawekezaji waliopo sekta ya utalii ili kubaini maeneo mapya yanayofaa kwa uwekezaji kwenye hifadhi hiyo.
Wajumbe wa Menejimenti ya NCAA wamefanya ziara ya kutembelea maeneo hayo yanayofaa kuwa uwekezaji katika huduma tofauti ikiwamo hoteli, kambi, utalii wa magari ya waya maeneo ya bonde la Ngorongoro na Embakai.
Chini ya uratibu wa Mpango wa matumizi bora (GMP), imeelezwa kwamba maeneo haya yataongeza makusanyo ya mapato kutokana na shughuli za utalii kwenye mamlaka ya hifadhi hiyo.
Akizungumza kwenye ziara hiyo Naibu Mhifadhi wa mamlaka hiyo Asangye Bangu alisema, ziara hiyo imelenga kuangalia maeneo yanayofaa kwa uwekezaji kama hoteli,kambi za muda za kulala wageni ,utalii wa baluni na biashara nyingine ndani ya hifadhi ikiwamo kuhakikisha wanakuwa na mpango endelevu wa uhifadhi,utalii na jamii inanufaika
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mawakala nchini (TATO), Wilbard Chambulo akizungumzia ushirikishwaji huo wa sekta binafsi aliipongeza Mamlaka hiyo kwa kushirikisha wadau waliopo kwenye sekta hiyo
Baadhi ya maeneo ambayo jopo hilo la wawekezaji liliyatembelea ni pamoja na nakumbusho ya Olduvai Gorge,Nasera rock,Ndutu na maeneo mengine.
Naibu
Mhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro Asangye Bangu
akizungumza na wafanyabiahara wawekezaji waliofanya ziara ya kujionea
maeneo mapya ya uwekezaji kwenye hifadhi hiyo.
Naibu
Mhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro (NCAA) Asangye
Bangu kulia, akizungumza na wafanyabiahara wawekezaji waliofanya ziara
ya kujionea maeneo mapya ya uwekezaji kwenye hifadhi hiyo.
Wawekezaji
na baadhi ya wafanyakazi wa Hifadhi ya Ngorongoro wakijadiliana baadhi
ya masuala ya utalii pembeni mwa kivutio cha mwamba wa Nasera Rock
kinavyopatikani hifadhin humo.
Mwenyekiti
wa Chama cha Mawakala wa Utalii nchini (TATO), Wilbard Chambulo
akiwaonyesha wawekezaji wenzake pamoja na maofisa wa Mamlaka ya Hifadhi
ya Ngorongoro baadhi ya maeneo yanayozunguka kivutio cha Nasera Rock.
Baadhi ya wawekezaji waliotembelea Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro wakimsikiliza Naibu Mhifadhji Asangye Bangu.
Naibu
Mhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro (NCAA) Asangye
Bangu kulia, akizungumza na viongozi wa Chama cha Mawakala wa Utalii
nchini (TATO) wakati wa ziara ya kutembelea na kujionea maeneo mapya ya
uwekezaji kwenye hifadhi hiyo.
Kundi
la wawekezaji wakimsikiliza Naibu Mhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya
Bonde la Ngorongoro Asangye Bangu wakati wa ziara yao ya kujionea maeneo
mapya ya uwekezaji.
No comments:
Post a Comment