HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, July 3, 2018

STARIMES YATOA OFA KABAMBE NDANI YA VIWANJA VYA SABASABA



Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Kampuni ya Startimes yawataka wananchi  kujitokeza kwa wingi kujipatia ofa kabambe katika banda lao lililopo ndani ya maonyesho ya 42 ya Kimataifa ya biashara kwenye Viwanja vya Sabasaba Jijini Dar es Salaam.

Hayo yamesemwa na Meneja Mahusiano wa Startimes Juma Suluhu Shalobalo alipozungumza na Globu ya Jamii na kuelezea ofa walizonazo ndani ya Viwanja vya Sabasaba ikiwemo punguzo la bei kwa Luninga na Ving'amuzi.

Mbali na hilo Juma amesema kuwa wana ofa nyingine kwa wananchi pindi wanapofika katika banda lao ambapo atakayepiga picha na kombe na kuiweka katika mitandao ya kijamii na na #kuhashtag basi atajipatia zawadi kutoka kampuni ya Startimes.
 Meneja Mahusiano wa Kampuni ya  Startimes Juma Suluhu Sharobaro akizungumza na Michuzi Blog kuhusu ofa walizozitoa ndani ya Sabasaba ikiwemo punguzo la bei kwa bidhaa zao pamoja na ofa kemkem kutoka katika banda lao la Maonyesho ya 42 ya Kimataifa ya Biashara ndani ya Viwanja vya Sabasaba Jijini Dar es Salaam.
  Mfanyakazi wa Kampuni ya Startimes Lulu Ibrahim akimuonyesha mteja namna ya kuperuzi kwenye simu kwa kumuonyesha APP ya Startimes inayopatikana katika simu za Smartphone zitakazomuwezesha mtumiaji kufuatilia vipindi vyote kiganjani kwake alipotembelea  banda lao ndani ya maonyesho ya 42 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea Kwenye Viwanja vya Sabasaba Jijini Dar Es Salaam.
 Mfanyakazi wa Kampuni ya Startimes Martha Masota akimuhudumia mteja alipotembelea  banda lao ndani ya maonyesho ya 42 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea Kwenye Viwanja vya Sabasaba Jijini Dar Es Salaam.
Mfanyakazi wa Kampuni ya Startimes Martin Emanuel akimuonyesha mteja aina ya king'amuzi kinachoweza kutumia Solar Energy alipotembelea  banda lao ndani ya maonyesho ya 42 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea Kwenye Viwanja vya Sabasaba Jijini Dar Es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad