HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, July 3, 2018

Naibu Waziri Shonza atoa wito kwa Wasanii Nchini kuhamasisha Utalii wa Ndani

 Naibu Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Idara  ya Utalii Hifadhi ya Taifa Ziwa Manyara Bibi. Eva Mallya (kulia) baada ya kuwasili katika  Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara (Lake Manyara National Park) ikiwa ni hatua ya kuhamasisha utalii wa ndani chini ya uratibu wa taasisi ya Tanzania Gospel Artist Network (TAGOANE)  Jijini Arusha.
 Naibu Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (wa kwanza kulia) akingalia ramani inayonyesha vivutio mbalimbali pamoja na wanyama wanaopatikana katika Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara jana Jijini Arusha  wakati wa ziara ya kutembele hifadhi hiyo, wengine ni Rais wa taasisi ya Tanzania Gospel Artist Network (TAGOANE) Dkt. Godwin Maimu (katikati) na kulia ni Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara Bibi. Noelia  Myonga.
 Naibu Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kulia) akipokea cover ya tairi la gari lenye nembo  ya  Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara kutoka kwa  Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara Bibi. Noelia  Myonga .
 Naibu Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (katikati) akisikiliza maelekezo  kutoka kwa Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara Bibi. Noelia  Myonga kuhusu chemchem ya maji moto ambayo inapatikana katika hifadhi  hiyo alipofanya ziara ya kuhamasisha utalii wa ndani kwa wasanii na watanzania kwa ujumla  lengo ni kuwa na utamaduni wa kutembelea vivutio hivyo .
  Naibu Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (katikati) akiangalia uoto wa asili ambao hupatikana katika Hifadhi ya Taifa ya  ya  Ziwa Manyara wakati wa ziara ya kutembelea hifadhi hiyo  hapo jana Jijini Arusha chini ya uratibu wa Taasisi ya Tanzania Gospel Artist Network (TAGOANE).
Naibu Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (katikati) akiwashukuru wasanii na wajasiriamali kutoka Jiji la Arusha ambao aliambatana nao katika ziara ya kuhamasisha  utalii wa ndani, iliyoratibiwa na Taasisi ya Tanzania Gospel Artist Network (TAGOANE) lengo ikiwa ni kuwajengea watanzania utamaduni wa kupenda kutembelea vivutio mbalimbali vilivyopo nchini ili kukuza uchumi wa nchi.  ( Picha na Lorietha Laurence-WHUSM,Arusha)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad