HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, July 6, 2018

BAADHI YA MAWAZIRI WATEMBELEA BANDA LA TRA KATIKA MAONYESHO YA SABASABA

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenister Muhagama akimsikiliza kwa makini Afisa Mwandamizi Uchambuzi Mifumo ya Biashara Mathias Chanila wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wakati Waziri huyo alipotembelea banda la TRA katika Maonyesho ya 42 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) ya mwaka 2018 yanayoendelea kufanyika jijini Dar es Salaam.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Mhandisi Stella Manyanya (kushoto) akitoa maoni yake kwa Afisa wa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Chama Siriwa (kulia) wakati Naibu Waziri huyo alipotembelea banda la TRA katika Maonyesho ya 42 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) ya mwaka 2018 yanayoendelea kufanyika jijini Dar es Salaam. Katikati ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenister Muhagama.
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akionyeshwa bili ya majengo na Meneja wa Huduma kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bi. Honester Ndunguru wakati Naibu Waziri huyo alipotembelea banda la TRA katika Maonyesho ya 42 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) ya mwaka 2018 yanayoendelea kufanyika jijini Dar es Salaam.
Mwanafunzi wa Kidato cha Sita kutoka Shule ya Sekondari St. Joseph Cathedral Tax Club iliyopo jijini Dar es Salaam Bertha Bureta akimuelezea Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji faida za kulipa kodi wakati Naibu Waziri huyo alipotembelea banda la Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika Maonyesho ya 42 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) ya mwaka 2018 yanayoendelea kufanyika jijini Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad