HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, June 11, 2018

ZIARA YA ULEGA JIMBO LA MKURANGA YAPAMBA MOTO, SEKTA YA ELIMU YAPEWA KIPAUMBELE

Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
MBUNGE wa Mkuranga na Naibu Waziri Ufugaji na Uvuvi Abdallah Ulega ameendelea na ziara yake katika jimbo la Mkuranga katika kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo na kusikiliza kero za wananchi wa jimbo hilo.

Akizungumza na wananchi wa jimbo hilo Ulega amesisitiza umoja na mshikamano  katika kuleta maendeleo katika jimbo hilo kwa mustakabali wa kizazi kijacho na amesema anatambua changamoto ambazo bado zinazikabili jimbo lao na ataendelea kupambana nazo.

Ulega amefafanua kuwa kuhusu maeneo yenye changamoto kama  miundombinu ya barabara kukatika baada ya mvua kupita tayari fedha zimetengwa kwa  maeneo hayo na kinachosubiriwa ni utekelezaji wa makandarasi.

Ulega amesisitiza kuwa ataendelea na jitihada zake na kushirikiana na wadau wa maendeleo katika  kupunguza kama si kumaliza kero ambazo bado zipo katika baadhi ya maeneo hasa katika  elimu, afya na masuala ya kijamii. 

Mkazi wa Mkuranga Yasin Ligwema ameeleza kuwa vyoo vipewe vipaumbele katika shule ili kuwaweka wanafunzi hasa watoto wa kike katika kujisitiri.

Aidha wananchi  wamempongeza Mbunge wao katika kutoa vipaumbele katika masuala ya maji, elimu na afya.

Ulega alihitimisha ziara hiyo kukabidhi zakatulfitry kwa wajumbe waliohudhuria.
 Naibu Waziri wa Mifungo na Uvuvi na Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega na Mbunge akisalimiana na wananchi wa kijiji cha Mlamleni katika mkutano huo.
 Sehemu ya wanachi wa kijiji cha Mlamleni  wakimsiliza Naibu Waziri wa Mifungo na Uvuvi, Abdullah Ulega na Mbunge wa Mkuranga  Abdallah Ulega  katika mkutano huo.
 Naibu Waziri wa Mifungo na Uvuvi na Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega  akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mlamleni juu ya kuendelea kushilikia na wanachi kwa kilijambo na kutatua kero zao.(picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii)
Mmoja wa wazee wa kijiji cha Mlamleni akielezea kero yake mbele ya Naibu Waziri wa Mifungo na Uvuvi na Mbunge wa Mkuranga,Abdallah Ulega.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad