HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, June 16, 2018

Maafisa TEHAMA Wakamilisha Mafunzo ya Mfumo Mpya wa Malipo (Epicor 10.2) Jijini Dodoma

Afisa TEHAMA, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bw. Robert Dudu (aliyesimama) akitoa maelekezo ya namna gani Afisa TEHAMA anatakiwa kutatua matatizo katika mfumo mpya wa malipo (epicor 10.2) wakati wa mafunzo ya mfumo huo kwa Maafisa TEHAMA kutoka Halmashauri za Mikoa ya Dodoma, Singida, Arusha, Shinyanga, Kigoma na Manyara, leo Jijini Dodoma.
Maafisa TEHAMA kutoka Halmashauri za Mikoa ya Dodoma, Singida, Arusha, Shinyanga, Kigoma na Manyara wakifuatilia mafunzo ya mfumo mpya wa malipo (epicor 10.2) leo, Jijini Dodoma.
Maafisa TEHAMA kutoka Halmashauri za Wilaya ya Kiteto, Hanang’ na Babati wakifanya mazoezi ya namna mfumo mpya wa malipo (epicor 10.2) unavyofanya kazi na namna gani ya kukabiliana na changamoto zitakazojitokeza katika mfumo huo pindi utakapoanza kutumika Julai 1 mwaka huu katika Halmashauri zote za wilaya, miji na majiji hapa nchini.
Maafisa TEHAMA kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mpwawa na Bahi wakifuatilia mafunzo ya mfumo wa malipo (epicor 10.2) ambayo yametolewa kwa Maafisa TEHAMA kutoka Mamlaka zote za Serikali za Mitaa ili kuwapa uelewa wa namna gani ya kutatua changamoto katika mfumo huo mara utakapoanza kutumika na Mamlaka hizo kuanzia Julai 1 mwaka huu.
Afisa TEHAMA kutoka Halmashauri ya Mji Shinyanga, Bw. Stanley Manyonyi na Afisa TEHAMA kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Bi. Swaumu Hamza wakiendelea na mafunzo ya mfumo mpya wa malipo (epicor 10.2) leo, Jijini Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad