HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, June 26, 2018

BIASHARA YA DAWA ZA KULEVYA ZISIPOKOMESHWA ATHARI KUBWA KUONGEZEKA

Biashara ya dawa za kulevya zisipokomeshwa na kuachwa ikaendelea nchini, athari zaidi  ikiwemo kuingiliwa kwa misingi ya kiutawala na wafanyabiashara wa dawa hizo kwa manufaa yao wao wenyewe binafsi zitaendelea kujitokeza kwani dawa za kulevya  limekuwa tatizo kubwa katika ulimwengu mkubwa na hata katika nchi ya Tanzania.
Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Jenista Mhagama ameyasema hayo, wakati wa kilele cha maadhimisho ya Kitaifa ya siku ya kupiga vita dawa za kulevya duniani iliyokwenda kwa kaauli mbiu ‘Tujenge Maisha yetu, Jamii yetu na Utu wetu bila Dawa za Kulevya’ iliyofanyika leo Mkoani Iringa.
Amesema matumizi na biashara ya dawa za kulevya yameendelea kusababisha madhara makubwa sana katika nchi ya Tanzania yakiwemo ya kiafya, madhara katika jamii inayotuzunguka, kiuchumi,  kimazingira, kisiasa na hata kiusalama.
Ameongeza kuwa matumizi ya dawa za kulevya ambayo kwa kiasi kikubwa watumiaji wake ni vijana yanaathari kubwa na hatari ya kupoteza nguvu kazi ya taifa letu hivyo, kwani wao ni tegemeo la taifa hasa katika kukuza uchumi na kuleta maendeleo endelevu, .matuimizi ya dawa za kulevya yasipopigwa vita na kuzuiliwa yataathiri uchumi wa nchi yetu, uzalishaji maadili, jamii na usalama kwa ujumla wa taifa letu.
“Mapambano  dhidi ya dawa za kulevya ni vita kubwa inayohitaji nguvu ya pamoja kwani madhara yake ni makubwa kwa jamii yetu hasa kwa vijana ambao ni nguvu kazi kwa taifa letu.., Ni ukweli usiopingika kuwa maendeleo ya usatawi wa taifa duniani  na hata katika nchi yetu yanategemea sana  nguvu kazi na hasa nguvu kazi ya vijana”, amesema Mhagama.
Pia amesema, mabinti wengi ambao wako katika umri wa, kusaidia kuongeza nguvu kazi katika nchi yetu wanakatishwa ndoto zao kwa kutumia dawa hizi na hata kupata madhara yanawasababishia matatizo mbali mbali jambo ambalo ni la kusikitisha sana
“Ni matarijio yangu kupitia maadhimisho haya ya siku ya leo wananchi wa mkoa wa Iringa, watakumbushwa na kuhamasishwa kushirikiana na serikali katika kupambana na vita hii kwani watumiaji wa dawa za kulevya ni watanzania wenzetu, tunaishi nao kila siku, ni vijana wetu tuliowazaa ni watoto wetu, hivyo ni wakati muafaka kwa kila mmoja wetu kusoma sheria kuhusu uuzaji utumiaji wa dawa za kulevya sambamba na ufahahamu wa athari za dawa hizo hapa nchini.
Amesema, kwa mujibu wa utafiti wa nguvu kazi wa mwaka 2014 inaonesha kuwa, nguvu kazi ya vijana wenye umri kati ya miaka 15 and 35 ni takribani watanzania  milioni 12.5 ambao ni sawa na asilimia 56 ya nguvu kazi yote ya nchi yetu.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mh. Jenista Mhagama akizungumza  na wananchi wa mkoa wa Iringa  wakati wa maadhimisho ya kitaifa ya siku ya kupambana na dawa za kulevya Duniani yaliyofanyika katika kiwanja cha Kichangani mkoani Iringa leo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad