HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, April 13, 2018

TPA YAWAKUTANISHA WA WADAU KWA LENGO LA KUFANYA TATHIMINI JUU YA KAZI ZAO

Naibu Waziri, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi na Mawasiliano), Atashasta Nditiye akizungumza kuhusu Serikali  ilivyojipanga kuhakikisha inachukua masoko ya kibandari katika nchi nane zinazoizunguka Tazania pamoja na kutenga dola milioni 400 za upanuzi wa kina cha bandari kuhakikisha meli kubwa zaidi zinaingia nchini na shehena za mizigo zinaongezeka wakati wa mkutano uliowakutanisha wadau mbalimbali kwa lengo la kufanya tathimini juu ya shughuli zinazofanywa na TPA.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi Bandari Tanzania (TPA), Deusdedit Kakoko akizungumza na wadau kuhusu bandari nyingi ambazo si rasmi kwa jina lingine zinaitwa bandari bubu kuwa kuna mpango kuzirasimisha bandari hizo ili zitambuliwe rasmi na kuchangia pato la taifa lakini pia tupunguze uingizwaji wa dawa za kulevya na bidhaa kinyemela nchini wakati wa mkutano uliowakutanisha wadau mbalimbali kwa lengo la kufanya tathimini juu ya shughuli zinazofanywa na TPA.
 Mkurugenzi wa Bodi ya Mamlaka ya Usimamizi Bandari Tanzania (TPA), Azizi Kilonge  akizungumza kuhusu ongezeko la tani Milioni sita za shehena kwa mwaka 2016 na kufikia tani Milioni 15 ni ishara tosha kuwa bandari inafanya vyema katika soko wakati wa mkutano uliowakutanisha wadau mbalimbali kwa lengo la kufanya tathimini juu ya shughuli zinazofanywa na TPA.
 Baadhi ya wadau pamoja na wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi Bandari Tanzania (TPA) wakimsikiliza Naibu waziri wakati wa mkutano uliowakutanisha wadau mbalimbali kwa lengo la kufanya tathimini juu ya shughuli zinazofanywa na TPA
Mgeni rasmi Naibu Waziri, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi na Mawasiliano), Atashasta Nditiye akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya mbalimbali pamoja na wafanyakazi wa TPA.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad