HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, March 20, 2018

MFANYABIASHARA APANDISHWA MAHAKAMA YA KISUTU KWA KUSAFIRISHA GRAMU 214 DAWA ZA KULEVYA


Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

Mfanyabiashara, Hariri Mohammed Hariri (45), mkazi wa Kinondoni, amepandishwa katika kizimba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kujibu Tuhuma za kusafirisha zaidi ya gramu 214 za dawa za kulevya.

 Akisoma hati ya mashtaka Wakili wa serikali, Clara Chalwe mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shaidi imedaiwa Machi 2 mwaka huu huko Kinondoni Matitu ndani ya Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam mshtakiwa alisafirisha dawa za kulevya aina ya Heroine Hydrochloride zenye uzito wa gramu 214.11.

 Hata hivyo, mshtakiwa hakuruhusiwa kujibu kitu chohote mahakamani hapo kwa kuwa Mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi za dawa za kulevy isipokuwa kwa kibali kutoka kwa DPP.

Kwa mujibu wa upande wa mashtaka, upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika. Na imeahirishwa hadi Aprili 4 mwaka huu

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad