HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, March 28, 2018

MABALOZI WA TANZANIA NCHINI RWANDA NA URUSI WAMUAGA MAKAMU WA RAIS TAYARI KWA KUELEKEA VITUO VYA KAZI

Balozi wa Tanzania Nchini Rwanda  Mhe.Ernest Mangu na Meja Jenerali Mstaafu Simon Marco Mumwi  wa  Urusi leo wamekutana na kuzungumza na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan mjini Dodoma.

Mabalozi hao walifika kwenye makazi ya Makamu wa Rais, Kilimani Dodoma  kwa lengo la kumuaga ,walimuahidi Makamu wa Rais kufanya kazi kwa ajili ya Tanzania.

Wamemuambia Makamu wa Rais wanajua dhamana kubwa waliopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na dhamira yake ya Tanzania ya Viwanda .
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Urusi Mhe. Jenerali Mstaafu Simon Marco Mumwi pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Rwanda Mhe. Ernest Mangu ambao walifika nyumbani kwa Makamu wa Rais kwa lengo la kumuaga kwenye makazi yake Kilimani mjini Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan(katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na  Balozi wa Tanzania nchini Urusi, Mhe. Jenerali Mstaafu Simon Marco Mumwi(kushoto) pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Rwanda, Mhe. Ernest Mangu(kulia) ambao walifika nyumbani kwa Makamu wa Rais kwa lengo la kumuaga kwenye makazi yake Kilimani mjini Dodoma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad