HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, February 22, 2018

RAIS MAGUFULI AHUDHURIA MKUTANO MAALUM WA WAKUU WA NCHI ZA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI (EAC) UNAOFANYIKA KAMPALA NCHINI UGANDA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia katika Mkutano huo Maalum wa Wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) unaofanyika Kampala nchini Uganda.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amesimama pamoja na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais wa Uganda Yoweri Museveni wa nne kutoka kulia, Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta pamoja na Rais wa Sudani ya Kusini Salva Kiir wakati Wimbo wa Jumuiya ya  Afrika Mashariki ulipokuwa ukipigwa katika ukumbi wa mkutano uliopo katika  eneo la Munyonyo Kampala nchini Uganda.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amekaa pamoja na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais wa Uganda Yoweri Museveni wanne kutoka kulia, Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta pamoja na Rais wa Sudani ya Kusini Salva Kiir wakati wa mkutano huo Maalumu wa Wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki unao endelea jijini Kampala.
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais wa Uganda Yoweri Museveni akifungua Mkutano huo maalum wa Wakuu wa nchi za Jumuiya ya  Afrika Mashariki Kampala nchini Uganda.
 Wajumbe kutoka nchi mbalimbali za Jumuiya a Afrika Mashariki wakifatilia hotuba mbalimbali katika Mkutano huo maalum.
  Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais wa Uganda, Yoweri Museveni katika picha na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli wa kwanza kulia, Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, pamoja na Rais wa Sudan ya Kusini Salva Kiir mara baada ya Mkutano  Maalum wa 19 wa Jumuiya hiyo uliofanyika  Kampala nchini Uganda.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Sudan ya Kusini, Salva Kiir kabla ya kuanza kwa mkutano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta kabla ya kuanza kwa mkutano huo wa 19 wa Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Kampala Uganda.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo  na Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta mara baada ya kupiga picha ya pamoja katika eneo la Munyonyo Kampala nchini Uganda.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wakati wakielekea kwenye ukumbi wa Mkutano Maalum wa Wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC unaojadili masuala mbalimbali ikiwemo Maendeleo ya Sekta ya Miundombinu na  Afya. PICHA NA IKULU

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad