HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, February 1, 2018

PROF. KAMUZORA ATEMBELEA NA KUKAGUA KITUO CHA OPARESHENI NA MAWASILIANO YA DHARURA.

Na. Mwandishi Wetu.
Katibu mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora ametembelea na kukagua kituo cha operesheni ya mawasiliano ya dharura na kujua maendeleo ya kituo hicho kilichopo Ofisi ya kanda Maalumu ya jeshi la Zima moto Jijini Dar es salaam.

Akitoa maelezo ya jinsi mradi huo unavyofanya kazi, Mratibu wa Taifa wa Mradi huo Alfei Daniel, alisema Mradi huo unafuatilia dharura za maafa nchini ikiwemo Ukame na Mafuriko umefadhiliwa na Mfuko wa Uhifadhi wa Mazingira Duniani UNDP, ambapo jukumu lake kubwa ni kukusanya taarifa za maafa na vyanzo vyake, kuchambua taarifa hizo, kuhamasisha, kufuatilia, kutoa tahadhari za awali na kuratibu dharura katika ngazi ya kitaifa.

Alfei alifafanua kwamba, mradi huo una vituo 36 tofauti nchini ambavyo vina wawezesha kupata taarifa popote walipo kupitia mtandao maalumu, unaosaidia kutoa tahadhari kwa wananchi wa eneo linalotarajiwa kupata maafa, ambapo mpaka sasa mradi umechukua mabonde mawili yaani bonde la Pangani na bonde la mto Ruvuma.

“Mfumo ambao umefungwa unaweza kutabiri na kutoa taarifa za maafa zinazo weza kutokea popote katika vituo hivyo kwa kutumia mtandao, kwa mfano kujaa kwa maji ambako kuna weza kupelekea mafuriko. Mfumo huu ukikamilika utaweza kuonyesha ramani na vituo vyake vyote vya hali ya hewa.” Alisema Alfei.

Aidha baada ya kupata maelezo ya mradi huo Prof. Kamuzora alishauri mradi huo ufanye jitihada kutoa elimu ya uokoaji kwa wanafunzi mashuleni na raia wote kwa ujumla, na kwa watu wasiokua na elimu ya uokoaji watahadharishwe kukaa mbali na matukio ya maafa kwani wengi wao huathirika au kupoteza maisha katika uokoaji kwa kukosa elimu hiyo.

“Ni lazima uongozi uhakikishe matumizi mazuri ya rasilimali za mradi huu na kuzuia uharibifu wa vifaa na fedha zinazotelewa na mashirika ya serikali na yasiyo ya serikali kuendesha mradi huu” Aliongeza Prof. Kamuzora.

Bw. Alfei alisisitiza kuwa mfumo huo unasaidia sana TMA katika kutabiri mabadiliko ya hali ya hewa kwa uhakika wa 87%, Wizara ya maji wanaweza kupata data kwa ajili ya kukuza vyanzo vya maji, vile vile hifadhi za taifa zinapata taarifa za hali ya hewa kwa urahisi kwa ajili ya kuhabarisha watalii na kujua mienendo ya wanyama, kwa ujumla huu mfumo unasaidia upatiknaji wa taarifa.

Mradi huu wa Uboreshaji wa Taarifa za Mabadiliko ya Tabia nchi na Mifumo ya utolewaji wa tahadhari za awali ulianza rasmi mwezi Januari, 2017 kwa dhumuni hasa la kuwezesha mawasiliano ya kujitahadhari na maafa,kujiandaa na maafa, na kipindi cha maafa ambapo mawasialiana ya haraka huitajika ili kuokoa maisha na makazi ya watu. Hivyo mradi huu umeundwa ili kuwezesha mawasialiano ya saa 24 kwa siku saba za wiki.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera naUratibu) Prof. Faustin Kamuzora akisaini kitabu cha wageni alipoenda kukagua kituo cha Mradi wa Uboreshaji wa Taarifa za Mabadiliko ya Tabia nchi na Mifumo ya utolewaji wa tahadhari za awali pembeni ni Kamanda wa Jeshi la zimamoto kanda maalumu Afande Peter Mabusi. Kituo hicho kipo  Ofisi ya kanda Maalumu ya jeshi la Zimamoto  jijini Dar es salaam.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora akisikiliza kwa makini maelezo kutoka kwa Mratibu wa Kitaifa wa Mradi wa Uboreshaji wa Taarifa za Mabadiliko ya Tabia nchi na mifumo ya utolewaji wa tahadahri za awali Alfei Daniel jinsi mfumo unavyotumika kupata taarifa za hali ya hewa na tahadhari za maafa kutoka vituo mbalimbali nchini vilivyowekwa mfumo huo.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora (katikati) akitoa ushauri kwa Kamanda wa Jeshi la zimamoto Kanda Maalumu  Afande. Peter Mabusi na Mratibu wa Kitaifa wa Mradi wa Uboreshaji wa Taarifa za Mabadiliko ya Tabia nchi na mifumo ya utolewaji wa taadhari za awali Alfei Daniel namna ya kuboresha huduma zao na mradi huo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad