Mwakilishi
wa TatuMzuka,Kemi Mutahaba akimkabidhi mfano wa hundi Bi Neema Mtewele
(38),ambaye ni mfanyabiashara wa nguo za akina mama Kariakoo jijini Dar
Es Salaam,aliyeibuka na kitita cha shilingi milioni 60 za TatuMzuka
mwishoni mwa wiki.
Neema
Mtewele (38),ambaye ni mfanyabiashara wa nguo za akina mama Kariakoo
jijini Dar Es Salaam,akifafanua mbele ya Waandishi wa habari (hawapo
pichani),namna alivyofanikiwa kushinda mamilioni hayo ya Mchezo wa
kubahatisha wa Tatumzuka.Neema alisema kuwa amekuwa akiucheza muda mrefu
mchezo huo bila mafanikio,lakini hakukata tamaa,alindelea kucheza na
hatimae akabahatika kuibuka mshindi wa milioni 60.
"Hizi
fedha kwakweli matumizi yake makubwa yatakuwa ni kuendeleza na
kuunyanyua zaidi mtaji wangu niliokuwa nao kwenye biashara yangu,bado
nahitaji kuikuza zaidi biashara yangu",alisema Neema huku akionesha
furaha ya wazi kwa kushinda kitita hicho cha milioni 60.
No comments:
Post a Comment