HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, January 11, 2018

VIONGOZI MBALIMBALI WAWAONGOZA MAELFU YA WAOMBOLEZAJI KWENYE MAZISHI YA MAMA PERAS NGOMBALE MWIRU, MAKABURI YA KINONDONI JIJINI DAR LEO

 Jeneza lenye mwili wa Marehemu Mama Peras Ngombale Mwiru (Mama Kinje), Mke wa Mmoja waasisi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mzee Kingunge Ngomale Mwiru ukiwasili kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam, alikopumzishwa kwenye nyumba yake ya milele. Mama Peras (Mama Kinje) amezikwa jioni ya leo kwenye makaburi Kinondoni, huku viongozi mbalimbali wa Kitaifa na Vyama vya siasa wakishiriki mazishi hayo.
 Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete akiwa na familia ya Marehemu, wakishuhudia Jeneza lenye mwili wa Mama Peras Ngombale Mwiru likishushwa kaburini, wakati wa mazishi yake yaliyofanyika jioni ya leo kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam. Kushoto kwake ni Mtoto wa Marehemu Mama Peras, Kinje Ngombale Mwiru aliyeambatana na mkewe.
 Mume wa Marehemu Mama Peras Ngombale Mwiru, Mzee Kingunge Ngombale Mwiru akiweka udongo kwenye kaburi ya Mke wake mpendwa, wakati wa mazishi yake yaliyofanyika jioni ya leo kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam.
 Mtoto wa Marehemu Mama Peras, Kinje Ngombale Mwiru na Mkewe Anitha wakiweka udongo kwenye kaburi la Mama yao. 
 Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete akiweka udongo kaburini.
Askofu akiweka msalaba kaburini.
 Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa na Mkewe Mama Regina wakiweka shada ya maua kwenye kaburi la Mama Peras Ngombale Mwiru (Mama Kinje), Mke wa Mmoja waasisi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mzee Kingunge Ngomale Mwiru
 Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba na Mkewe wakiweka shada ya maua kwenye kaburi la Mama Peras Ngombale Mwiru (Mama Kinje), Mke wa Mmoja waasisi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mzee Kingunge Ngomale Mwiru
Mama Anna Mkapa akiweka shada ya maua kwenye kaburi la Mama Peras Ngombale Mwiru (Mama Kinje), Mke wa Mmoja waasisi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mzee Kingunge Ngomale Mwiru.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad