HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, January 10, 2018

ULEGA AMEWAAGIZA WATENDAJI NGAZI YA WILAYA NA MKOA KUSIMAMIA ZOEZI LA UPIGAJI CHAPA MIFUGO

Serikali imewataka  watendaji   ngazi  ya   wilaya  na  mkoa  kusimamia kwa umakini zoezi  la  upigaji  chapa   mifungo  linaloendea hapa nchini.

Agizo hilo amelitoa Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah   Ulega wakati alipokuwa anazungumza na baadhi ya watendaji  wa mkoa wa Lindi kwenye ziara  yake ya kikazi  ya siku mbili  mkoani humo.

Ulega  alisema mtendaji  yeyote  atakaye bainika kukwamishwa  zoezi hilo  hata vumiliwa  na kueleza kuwa kuna baadhi    wanaonekana kukwamisha zoezi hilo kwa madai ya kukosa  bajeti ya kuendesha zoezi.

Wapo watendaji wanaodharau zowezi hili kwa kweli serikali haita waacha salama  alisema   Ulega.

Kwa upande  wake  mkuu wa mkoa wa Lindi  Godfrey Zambi  amesema kuwa kunachangamoto kadha zilizosababisha  baadahi  ya  Halmshauri kushindwa kutekeleza  jukumu  hilo  kwa wakati.

Zambi alisema   Halmshuari  ya wilaya Ruangwa ngo’mbe  268 kati  3000  wamepigwa chapa wakati wilaya   ya  Nachingwea  ngombe  328 tayari wamekamilisha zoezi  hilo.
 Naibu Waziri wa Mifungo na Uvuvi ,Abdallah Ulega na akizungumza na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Lindi mara baada ya kupokea  ripoti ya ya mkoa huo.
 Naibu Waziri wa Mifungo na Uvuvi ,Abdallah Ulega akizindua zowezi la upigaji chapa mifugo katika mkoa wa Lindi.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii Lindi.

Naibu Waziri wa Mifungo na Uvuvi ,Abdallah Ulega akizungumza na  viongozi mbalimbli,wafungaji  juu ya  kuhamasisha zowezi la ubikaji chapa mifugo mkoa wa Lindi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad