HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, January 17, 2018

MBUNGE NJALU AFANYA HARAMBEE YA UJENZI WA SHULE SIMIYU.

Mbunge wa jimbo la Itilima Mkoani Simiyu Njalu Daudi Silanga akiweka jiwe la msingi katika ujenzi wa shule ya ITUBILO PRE &APRIMARY MEDIUM SCHOOL lililojengwa kwa mfuko wa kanisa mmara baada ya kumaliza ibda ya pamoja na waumini wa kanisa hilo, Pembeni ni Mchungaji wa kanisa la SDA Itubilo Michael Phabian.



Na Mwandishi wa Globu, Simiyu.

Mbunge wa jimbo la Itilima Mkoani Simiyu Njalu Daudi Silanga ameshiriki ibaada katika kanisa la SDA liliopo Kijiji cha Itubilo na kufanya harambee ya uchangiaji wa ujenzi ya shule ya  Itubilo Pre & Primary Medium School  na kuhamasisha wananchi kujitokeza na kusaidia kwenye ujenzi huo.


Njalu ambaye alikuwa mgeni ramsi kwenye harambee hiyo, aliweza kuzungumza na wanakijiji wa Itubilo na kuwataka wafahamu kuwa msingi mkubwa wa urithi kwa mtoto ni elimu na zaidi wanakijiji washirikiane kwa pamoja kuhakikisha wanafanikisha ujenzi wa shule hiyo itakayokuja kuwa na manufaa kwa vizazi vya baadae.

Wakati wa uendeshaji wa jarambee hiyo, Njalu aliweza kuchangia kiasi cha fedha shilling milioni moja na laki tano (1,500,000) pamoja na mifuko ya saruji 170 ili kuongeza nguvu ya ujenzi wa kanisa hilo.

Wazee wa Kanisa kwa pamoja waliweza kumshukuru Mbunge wao Njalu kwa hatua kubwa aliyofanya ya kuwapatia mifuko ya saruji ambapo wanaamini kuwa wataitumia kuendeleza ujenzi wa shule hiyo itakayokuwa ni kuanzia elimu ya  awali na Msingi. 


Mbunge wa jimbo la Itilima Mkoani Simiyu Njalu Daudi Silanga akizungumza na waumini wa Kanisa la SDA Itubilo pamoja na wanakijiji baada ya kumaliza ibada ya pamoja na kuweka jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Itubilo Pre & Primary Medium School na kuchangia kiasi cha shillingi milioni moja na laki tano (1,500,000) na mifuko ya saruji 170 kwa ajili ya ujenzi wa shule.

Mbunge wa jimbo la Itilima Mkoani Simiyu Njalu Daudi Silanga akivalishwa skafu na Vijana wa pathfinder mara baada ya kuwasili katika kanisa ;a SDA lililopo Kijiji cha Itubilo kata ya Lugulu tarafa ya Kinamweli.


Mbunge wa jimbo la Itilima Mkoani Simiyu Njalu Daudi Silanga akiwa anapokea mkono wa shukrani kutoka kwa Mzee wa kanisa Enock Maduhu mara baada ya kuchangia kiasi cha fedha shillingi 
milioni moja na laki tano (1,500,000)

 na mifuko ya saruji 170 kwa ajili ya ujenzi wa shule.
Mbunge wa jimbo la Itilima Mkoani Simiyu Njalu Daudi Silanga akiwa anajadiliana jambo na Mwalimu Abel Pondela wakati wa harambee ya uchangiaji hela ya ujenzi wa shule ya Itubilo Pre & Primary Medium School na kuchangia kiasi cha shillingi 
milioni moja na laki tano (1,500,000)

 na mifuko ya saruji 170 kwa ajili ya ujenzi wa shule.
Mbunge wa jimbo la Itilima Mkoani Simiyu Njalu Daudi Silanga akifuatilia jambo sambamba na wanakijiji wa Itubilo wakati wa harambee ya uchangiaji ya ujenzi wa shule ya Itubilo Pre & Primary Medium School na kuchangia kiasi cha shillingi 
milioni moja na laki tano (1,500,000)

 na mifuko ya saruji 170 kwa ajili ya ujenzi wa shule.





No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad