HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, January 11, 2018

KIGWANGALA ATAKA KAULI MBIU YA KUTANGAZA UTALII

Na Said Mwishehe
WAZIRI wa Maliasili na Utalii Dkt.Hamis Kigwangala amesema ipo haja ya kuwa na kauli mbiu ambayo itatumika kuutangaza utalii wa Tanzania katika mataifa mbalimbali duniani.

Amesema Tanzania imejaaliwa kuwa na maeneo mengi ya utalii lakini hayajafahamika kutokana na nguvu ndogo ya kuyatangaza kwake, hivyo kusababisha watalii wengi kufanya utalii katika maeneo machache ya utalii ukiwamo Mlima Kilimanjaro.

Dk.Kigwangala ametoa kauli hiyo jijini  Dar es Salaam leo wakati anazindua Kamati ya Utambulisho wa Utalii Tanzania na kufafanua kuna vivutio vingi na sasa ipo haja kuendelea kuvitangaza kwa nguvu zote.

Amesema wajumbe wa kamati watakuwa na jukumu la kuweka mikakati sahihi ya kuhakikisha utalii wa Tanzania unaendelea kutangazwa kwa lengo la kuongeza watalii wa ndani na nje ya nchi.

"Tunayo maeneo mengi ya utalii lakini yanayofahamika ni machache, kuna watalii wanakuja kwa ajili ya kwenda Mlima Klimanjaro na wengine Mbuga ya Serengeti wakati yapo maeneo mengi ya utalii.Lazima tutangaze utalii wetu na hii kamati itatusaidia kutuongoza,"amesema Dk.Kigwangala.

Amewataka wajumbe wa kamati hiyo kutafuta kauli mbiu ambayo itautangaza utalii wa Tanzania nchi mbalimbali duniani.

"Iwe kauli mbiu ambayo itatutofautisha Tanzania na nchi nyingine kwenye mambo ya utalii na lazima tuwe na kauli mbiu ya kipekee katika kuutangaza utalii wetu,"amesema Dk.Kigwangala.

Amefafanua kuna mbuga za wanyama 16 lakini zinazotambulika chache,hivyo juhudi zinahitaji kutangaza vivuto vya utalii vilivyopo.

Mwenyekiti Mwenza wa Kamati ya Kitaifa ya Utambulisho wa Utalii Tanzania Richard Lugimbana amemhakikishia Dk.Kigwangala kuwa wanatambua jukumu ambalo wamepewa na hivyo ni wajibu wao kuweka mikakati ambayo itasaidia kuutambulisha utalii wetu. 

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Utalii Devotha Mdachi amefafanua kamati hiyo ina jumla ya wajumbe 21 ambao wengi wao ni  watalaamu wa masoko.

Ameongeza utambulisho mpya kwa ajili ya kutangaza utalii wa Tanzania utaifanya nchi kuwa katika ramani nzuri ya kutambulika kwa vivutio vyake vya utalii.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Khamis Kigwangalla akisisistiza jambo wakati wa hafla ya uzinduzi wa Kamati ya Kitaifa ya Utambulisho wa Utalii wa Tanzania leo hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Utalii Jijini Dar es Salaam leo. Kamati hiyo yenye wajumbe 22 imeundwa na Mhe. Waziri kwa lengo la kupitia na kubuni mkakati mbadala wa namna ya kutangaza utalii wa Tanzania ndani na nje ya nchi.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Utambulisho wa Utalii wa Tanzania Bibi. Devotha Mdachi akielezea jambo mbele ya wajumbe wa kamati hiyo (hawapo pichani) mara baada ya kuzinduliwa rasmi kwa Kamati hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti Mwenza wa Kamati hiyo Richard Rugimbana. Kamati hiyo yenye wajumbe 21imeundwa na Mhe. Waziri kwa lengo la kupitia na kubuni mkakati mbadala wa namna ya kutangaza utalii wa Tanzania ndani na nje ya nchi.
 Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Kitaifa ya Utambulisho wa Utalii wa Tanzania wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Khamis Kigwangalla wakati wa hafla ya uzinduzi wa kamati hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Kamati hiyo yenye wajumbe 21 imeundwa na Mhe. Waziri kwa lengo la kupitia na kubuni mkakati mbadala wa namna ya kutangaza utalii wa Tanzania ndani na nje ya nchi.
Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Khamis Kigwangalla (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya Kitaifa ya Utambulisho wa Utalii wa Tanzania lmara baada ya uzinduzi wa kamati hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Kamati hiyo yenye wajumbe 21 imeundwa na Mhe. Waziri kwa lengo la kupitia na kubuni mkakati mbadala wa namna ya kutangaza utalii wa Tanzania ndani na nje ya nchi.
Picha na Frank Shija – MAELEZO

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad