HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, December 24, 2017

MPINA AAGIZA MKATABA WA OVENCO KUVUNJWA NA KUUNDWA KWA MKATABA MPYA.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina ameagiza kuvunjwa kwa mkataba ulioundwa baina ya RANCHI ya Taifa NARCO na kampuni ya Overland  kwa pamoja na kuunda kampuni ya OVENCO uliyokuwa na mapungufu ya kisheria na kiutendaji kufunjwa ifikapo mwisho wa mwezi huu wa December na kutoa mwezi mmoja kwa  NARCO kuunda mkataba mpya wenye mwongozo wa kisheria.
Mpina aliyasema hayo jana alipokuwa katika ziara ya ukaguzi wa Ranchi ya Mzeri iliyopo wilayani Handeni Mkoani Tanga yenye ukubwa kwa Hekta 41,000  ambapo hekta 21,000 zinamililiwa na Muwekezaji kampuni ya Overland muwekezaji ambaye, amekuwa na mgogoro wa muda mrefu na  NARCO ambapo baada ya Waziri Mpina kusililiza pande zote mbili na kujiridhisha  na kumuona muwekezaji kutokuwa na uwezo wa kufikia malengo ya kuendeleza eneo lote la ardhi  ambalo amekuwa akiliendeleza bila makubaliano yoyote ya kisheria, jambo ambalo limempelekea Waziri Mpina kuagiza  NARCO  kuingia katika hatua ya kuunda mkataba mpya baina yake na muwekezaji huyo utakaozingatia masharti mapya ya kisheria ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa muwakilishi wa NARCO Katika kitalu hicho.
Aidha Waziri Mpina ameagiza muwekezaji huyo asihamishwe kwa kuwa ameonyesha nia ya kuendeleza eneo hilo kwa kuwepo kwa ng’ombe wambegu aina ya Borani pamoja na miundombinu mingine
Akizungumzia eneo la hekta 20,000 linalomilikiwa na wawekezaji wengine wadogo, Mpina aliwataka wawekezaji hao kulipa na kumaliza madeni yote ya kodi ya serikali wanayodaiwa  katika vitalu vyao ifikapo January mosi 2018.
“Wawekezaji wengine wengine wanaomiliki vitalu katika ranchi hii ya Mzeri mnatakiwa kulipa madeni yote ya kodi mnayodaiwa na Serikali kodi mnayolipa ya shilingi elfu moja (1000) kwa mwaka ni kidogo sana lakini bado hamlipi, kinyume na hili ni bora muondoke wenyewe au tutawaondosha kwa nguvu muda huo ukifika. “ Alisisitiza Mpina.
“Baada ya kumaliza kulipa nawagiza NARCO kuwapa miezi mitatu wawekezaji hawa kuhakikisha wanaweka miondombinu inayolingana na ukubwa wa eneo na matumizi ya ardhi , tunataka wawekezaji wafikie malengo na mashamba haya yafanye kazi.” Alisema Mpina.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Handeni Godwin Gondwe alisema kuwa, Wiaya ya handeni itaendelea kulinda  mazao na rasilimali za Mifugo kupitia sheria ndogondogo ambazo wilaya hiyo imejiwekea.
Akizungumza kwa namna ambavyo ameyapokea maagizo wa Waziri Mpina , mmiliki wa kampuni ya Overland Bw. Faisal Edha alisema kuwa amekubalina na maagizo ya Mpina na yupo tayari kuendelea na uwekezaji na anaamini kuwa mkataba mpya utanufaisha pande zote mbili.
Awali akipokea taarifa ya Mifugo ya wilaya ya Handeni, Waziri Mpina alimpongeza Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Godwin Gondwe  kwa kuzitambua sheria za usimamizi wa mifugo na kuzitumia jambo ambalo litasaidia kwa kiasi kikubwa kutokuwepo kwa uonevu kwa watu wa jamii ya wafugaji na kuzitaka wilaya nyingine nchini kuiga mfano wa wilaya hiyo kwa kuunda sheria ndogo ndogo zitakazowaongoza katika sekta  ya mifugo.
 Katikati Waziri wa Mifugo na Uvuvi. Mhe. Luhaga Mpina akiongea  vyombo vya habari baada ya ziara ya ukaguzi wa  baadhi ya vitalu katika Ranchi ya Mzeri iyopo Wilayani Handeni Mkoani Tanga, kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Handeni Godwin Gondwe, na kulia ni mkurugenzi wa kampuni ya Overland Bw. Faizal Edha.
Ng’ombe aina ya Borani inayomilikwa na muwekezaji kampuni ya Overland katika Ranchi ya Mzeri , Wilayani Handeni Mkoani Tanga.
 Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina kati kati na Mkuu wa Wilaya ya Handeni kulia Godwin Gondwe pamoja na wataalam kutoka Wizarani na Mkoani Tanga wakiwa katika zoezi la kukagua baadhi ya vitalu  vilivyopo katika Ranchi ya Mzeri Wilayani Handeni.
Aliyesinama wa pili kulia ni Waziri wa Mifugo na uvuvi Luhana Mpina, kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Handeni Godwin Gondwe wakiangalia sehemu ya kunyweshea ng’ombe maji katika ranchi ya Mzeri wilayani Handeni.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad