HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, December 6, 2017

ECOBANK YABORESHA MIUNDOMBINU YA MAJI SHULE YA MSINGI HANANASIFU JIJINI DAR

Shule ya Msingi Hananasifu, iliyopo katika manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, imeepukana na dhahama ya kuweza kupata magonjwa ya mlipuko kama vile Kipindupindu baada ya Ecobank kuboresha miuondombinu ya maji shuleni hapo.
Kifuatia uwekwaji wa miundombinu hiyo bora pia, Ecobank imeweka tanki maalumu ili kurahisisha usambazaji pamoja na upatikanaji wa Huduma ya maji safi na salama  katika vyoo na maeneo mbali mbali shuleni hapo yenye uhitaji wa maji kwa wanafunzi na walimu.
Aidha benki hiyo imetoa vitabu pamoja na kukabidhi zawadi mbali mbali kwa wanafunzi wa darasa la kwanza hadi la sita walioshika nafasi ya kwanza hadi ya tatuu
Akizungumza wakati wa hafla ya kufungua Kisima hicho leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi mtendaji wa Ecobank, Mwanahiba Mzee amesema,  msaada huo utasaidia shule hiyo kupata maji safi na salama na dhamira yao kubwa ni kuunga mkono juhudi za serikali za kuinua kiwango cha elimu  nchini kwa kuboresha miundombinu.
"Tuliguswa sana baada ya kupewa taarifa kuwa shule hii inawanafunzi 728 lakini miundombinu ya maji imeziba na kubakia sehemu moja tu ambayo inatumiwa na shule nzima, vyoo havina maji na hivyo imekuwa changamoto ya kiafya kwa wanafunzi na walimu, tukaona in vyema kusaidia na kuokoa afya za watoto, amesem Mzee.
Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Aiddah Uisso amesema walikuwa wakikabiliwa na chanhamoto kubwa ya maji kwani kwa idadi kubwa ya wanafunzi waliopo shuleni hapo, huduma ya maji na salama ni muhimu sana.
" Kwa msaada wa maboresho ya miundombinu yaliyofanyika kwa sasa tunuhakika wa maji safi na salama kwa walimu na wanafunzi.  Vitabu  pamoja na zawadi vilivyotolewa kwa wanafunzi bora, kutaongeza hamasa kwao kufanya vizuri zaidi.
 Mkurugenzi wa Mtendaji Wa Ecobank Tanzania, Mwanahiba Mzee akikata utepe kuashiria kumaliza uwekaji wa miundombinu ya maji safi na salama kwa kukabidhi mabomba yaliyojengwa katika  shule ya Msingi Hananasifu, kulia mwenye nguo nyeusi ni Mwalimu Mkuu Wa Shule hiyo, Aida Uisso wakishuhudiwa na baadhi wa ya wafanyakazi wa benki hiyo, walimu na wanafunzi.
 Mkurugenzi wa Mtendaji Wa Ecobank Tanzania, Mwanahiba Mzee akizungumza na walimu pamoja na wafanyakazi wa Benki hiyo baada ya kumaliza uwekaji wa miundombinu bora na tanki maalumu la maji katika shule hiyo ili kurahisisha usambazaji na upatikanaji wa maji safi na salama shuleni hapo. Pembeni yake ni Afisa Elimu manispaa ya Kinondoni, Mikidadi Azizi akifuatiwa na Diwani wa kata ya Hananasifu, Ray Kimbita.
 Mkurugenzi wa Mtendaji Wa Ecobank Tanzania, Mwanahiba Mzee (kulia) akikabidhi msaada wa vitabu vya kiada kwa Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi ya Hananasifu, Aida Uisso iliyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Wanafunzi wa shule ya Msingi ya Hananasifu iliyopo katika manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, darasa la kwanza hadi la sita waliofanya vizuri katika mitihani yao wakiwa wameshikilia zawadi zao walizozawadia na Ecobank kwa ufaulu huo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad