HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, November 23, 2017

RAIS MAGUFULI MGENI RASMI UZINDUZI WA HOSPITALI YA TAALUMA MUHAS KAMPASI YA MLOGANZILA

 Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Prof. Appolinary Kamuhabwa akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu uzinduzi wa Hospitali ya Taaluma na Tiba ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili - MUHAS Kampasi ya Mloganzila leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Huduma za Hospitali Prof. Said Abood na Afisa Habari wa Idara ya Habari (MAELEZO) Jonas Kamaleki. Uzinduzi huo utafanyika tarehe 25 Novemba 2017 ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
 Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) anayeshughulikia Huduma za Hospitali Prof. Said Abood akifafanua jambo mbele ya  Waandishi wa Habari kuhusu uzinduzi wa Hospitali ya Taaluma na Tiba ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili - MUHAS Kampasi ya Mloganzila leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili (MUHAS) Prof. Appolinary Kamuhabwa na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya dharura Dk. Hendry Sawe. Uzinduzi huo utafanyika tarehe 25 Novemba 2017 ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli. 
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya dharura wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Dk. Hendry Sawe akielezea jambo mbele ya  Waandishi wa Habari kuhusu uzinduzi wa Hospitali ya Taaluma na Tiba ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili - MUHAS Kampasi ya Mloganzila leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Afisa Habari wa Idara ya Habari (MAELEZO) Jonas Kamaleki, Kaimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili (MUHAS) Prof. Appolinary Kamuhabwa na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) anayeshughulikia Huduma za Hospitali Prof. Said Abood. Uzinduzi huo utafanyika tarehe 25 Novemba 2017 ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli. (Picha na: Frank Shija - MAELEZO)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad