HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, November 15, 2017

PESAPAL WAZINDUA MPANGO MPYA WA KUTUMIA MALIPO KWA NJIA YA PESAPAL SABI

 Pesapal leo imetangaza kuzindua suluhisho/mpango wake wa uuzaji kwa kutumia simu na kuipa jina la “Pesapal Sabi”. Sabi inaruhusu watu mbalimbali na wafanyabiashara kufanya malipo salama kwa kutumia kadi kwenye duka kwa kutumia simu yake ya mkononi ya android au kompyuta kibao (tablet) kwa wakati ambao mtu anakuwa na kazi nyingi na kushindwa kufika dukani kwa muda huo.
Pesapal inapatikana Uganda, Kenya na Tanzania. Bidhaa hii inalenga kusaidia wafanyabiashara kwa kutumia njia ya simu pekee na (SMES) wafanyabiashara wadogo na wa kati, hadi wauzaji wa eneo kubwa Zaidi kufanya malipo ya kadi kwa ufanisi Zaidi. Kwa sasa Sabi inauwezo wa kutumia visa na ‘mastercard’ katika kadi za mikopo na kadi za matumizi katika sarafu zote za ndani na kwa dola za kimarekani.

Malipo haya kwa kutumia kadi yatakuwa yakifanywa kwa njia ya ‘Bluetooth’ kupitia katika kifaa cha Sabi mpos kinachotolewa na Pesapal. Kifaa hiki cha sabi kina uwezo wa kuhamishika kutoka katika eneo moja kwenda jingine na kina uwezo wa mauzo Zaidi ya 250 kwa mara moja. Kifaa hiki kina uwezo wa kufanya malipo ya chip na pin vile vile kwa kutumia njia ya NFC ‘malipo bila kuwasiliana’ (contactless payments). Wamiliki wa biashara pia watakuwa na uwezo wa kuangalia historia za mauzo yao na kutoa risiti za malipo kwa kutumia Sabi katika simu zao za Android.

Matoleo ya baadae ya Sabi yatakuwa na uwezo wa kutumia “kusapoti” MVISA. M-PESA na malipo ya kadi ya Marekani (American express payments) yatakayoongezwa katika chaguzi za malipo wafanyabiashara watakayotoa kwa wateja wao.

Kwa kuanzia Pesapal inatoa suluhisho la malipo ya mtandaoni (malipo kwa njia ya mtandao), lakini pia imeongeza sabi katika bidhaa zake za biashara. Tunawezesha wafanyabiashara wadogo kuweza kuitikia kwa njia za malipo zinazopendwa na wateja wao.

Akizungumza juu ya Sabi Afisa Mtendaji mkuu wa Pesapal Agosta Liko alisema, “Tumekuwepo ili kuimarisha/ kuweka uimara wa kifedha na kiuchumi katika soko ambalo tupo. 
Tunatoa uhuru katika biashara waweze kufikia huduma ambazo zilikuwa na changamoto katika upatikanaji wake ama ni kutokana na ukubwa au kiasi. 

Na Sabi tunafanya hivyo katika njia inayofikiwa kwa urahisi, nafuu, na ni njia ya simu inayopatikana mahali popote. Hii pia ni njia yetu ya kupeleka huduma za kifedha katika sekta zisizo rasmi, sehemu ambazo awali zilikuwa hazijahifadhiwa. Tutalenga hasa katika miji ya Dar es salaam, Arusha, na Zanzibar, kwa kuanzia na baada ya hapo tutaendelea kusambaa katika sehemu zingine mbalimbali kulingana na kukua kwa soko.

Wafanyabiashara/ biashara wanaweza kuifikia sabi kwa njia ya mtandao kupitia https://www.pesapal.com  ambapo watatengezeza/ wataanda akaunti ya biashara na kusaini mkataba wa mfanyabiashara (merchant contract). Kisha wataendelea kununua na kupata huduma zao za sabi punde tu zitakapofikishwa, zitaandaliwa kwa ajili yao na kuwawezesha kuanza kutumia ndani ya masaa 24.

Pesapal kwa jumla ni PCI PIN na PCI DSS ambayo imethibitishwa, maana yake ni kwamba viwango vya usalama wa kimataifa vinatumiwa kwa shughuli zote za kimapato za kadi ili kuhakikisha usalama kwa wafanyabiashara na wateja wao.


KUHUSU PESAPAL LTD.
Ilianzishwa mwaka 2010, Pesapal hutoa njia rahisi, salama na kwa watu binafsi na biashara
kufanya na kukubali malipo katika Afrika. Malipo ya Pesapal hufanya kazi kwenye mtandao na moja kwa moja kwenye simu.

Vipengele vingi katika utaratibu wa pesapal vinalenga kulinda wanunuzi na wauzaji wetu kwa kuwapa nafasi ya kuthibitisha ubora wa bidhaa na huduma kabla ya kutoa malipo

Pesapal wanashirikaina na mabenki, waendeshaji wa mitandao ya simu na makampuni yanayotoa kadi za mikopo ili kuwapatia wateja/watumiaji fursa nyingi iwezekanavyo katika kufanya malipo. Kwa wafanyabiashara, tunawapatia  muda wa makubaliano kwa malipo yoyote katika akaunti ya benki waliyochagua.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad