Pesapal leo imetangaza kuzindua suluhisho/mpango wake wa uuzaji kwa kutumia simu na kuipa jina la “Pesapal Sabi”. Sabi inaruhusu watu mbalimbali na wafanyabiashara kufanya malipo salama kwa kutumia kadi kwenye duka kwa kutumia simu yake ya mkononi ya android au kompyuta kibao (tablet) kwa wakati ambao mtu anakuwa na kazi nyingi na kushindwa kufika dukani kwa muda huo.
Pesapal
inapatikana Uganda, Kenya na Tanzania. Bidhaa hii inalenga kusaidia
wafanyabiashara kwa kutumia njia ya simu pekee na (SMES) wafanyabiashara wadogo
na wa kati, hadi wauzaji wa eneo kubwa Zaidi kufanya malipo ya kadi kwa ufanisi
Zaidi. Kwa sasa Sabi inauwezo wa kutumia visa na ‘mastercard’ katika kadi za
mikopo na kadi za matumizi katika sarafu zote za ndani na kwa dola za
kimarekani.
Malipo
haya kwa kutumia kadi yatakuwa yakifanywa kwa njia ya ‘Bluetooth’ kupitia
katika kifaa cha Sabi mpos kinachotolewa na Pesapal. Kifaa hiki cha sabi kina
uwezo wa kuhamishika kutoka katika eneo moja kwenda jingine na kina uwezo wa
mauzo Zaidi ya 250 kwa mara moja. Kifaa hiki kina uwezo wa kufanya malipo ya
chip na pin vile vile kwa kutumia njia ya NFC ‘malipo bila kuwasiliana’
(contactless payments). Wamiliki wa biashara pia watakuwa na uwezo wa kuangalia
historia za mauzo yao na kutoa risiti za malipo kwa kutumia Sabi katika simu
zao za Android.
Matoleo
ya baadae ya Sabi yatakuwa na uwezo wa kutumia “kusapoti” MVISA. M-PESA na
malipo ya kadi ya Marekani (American express payments) yatakayoongezwa katika
chaguzi za malipo wafanyabiashara watakayotoa kwa wateja wao.
Kwa
kuanzia Pesapal inatoa suluhisho la malipo ya mtandaoni (malipo kwa njia ya
mtandao), lakini pia imeongeza sabi katika bidhaa zake za biashara. Tunawezesha
wafanyabiashara wadogo kuweza kuitikia kwa njia za malipo zinazopendwa na
wateja wao.
Akizungumza
juu ya Sabi Afisa Mtendaji mkuu wa Pesapal Agosta Liko alisema, “Tumekuwepo ili
kuimarisha/ kuweka uimara wa kifedha na kiuchumi katika soko ambalo tupo.
Tunatoa uhuru katika biashara waweze kufikia huduma ambazo zilikuwa na
changamoto katika upatikanaji wake ama ni kutokana na ukubwa au kiasi.
Na Sabi
tunafanya hivyo katika njia inayofikiwa kwa urahisi, nafuu, na ni njia ya simu
inayopatikana mahali popote. Hii pia ni njia yetu ya kupeleka huduma za kifedha katika sekta zisizo rasmi, sehemu
ambazo awali zilikuwa hazijahifadhiwa. Tutalenga hasa katika miji ya Dar es
salaam, Arusha, na Zanzibar, kwa kuanzia na baada ya hapo tutaendelea kusambaa
katika sehemu zingine mbalimbali kulingana na kukua kwa soko.
Wafanyabiashara/
biashara wanaweza kuifikia sabi kwa njia ya mtandao kupitia https://www.pesapal.com ambapo
watatengezeza/ wataanda akaunti ya biashara na kusaini mkataba wa mfanyabiashara
(merchant contract). Kisha wataendelea kununua na kupata huduma zao za sabi
punde tu zitakapofikishwa, zitaandaliwa kwa ajili yao na kuwawezesha kuanza
kutumia ndani ya masaa 24.
Pesapal kwa jumla ni PCI PIN na PCI DSS ambayo
imethibitishwa, maana yake ni kwamba viwango vya usalama wa kimataifa vinatumiwa kwa shughuli zote za
kimapato za kadi ili kuhakikisha usalama kwa wafanyabiashara na wateja wao.
KUHUSU PESAPAL LTD.
kufanya na kukubali malipo katika Afrika.
Malipo ya Pesapal hufanya kazi kwenye mtandao na moja kwa moja kwenye simu.
Vipengele vingi katika utaratibu wa pesapal
vinalenga kulinda wanunuzi na wauzaji wetu kwa kuwapa nafasi ya kuthibitisha
ubora wa bidhaa na huduma kabla ya kutoa malipo
Pesapal wanashirikaina na mabenki,
waendeshaji wa mitandao ya simu na makampuni yanayotoa kadi za mikopo ili
kuwapatia wateja/watumiaji fursa nyingi iwezekanavyo katika kufanya malipo. Kwa wafanyabiashara, tunawapatia
muda wa makubaliano kwa malipo yoyote katika akaunti ya benki
waliyochagua.
No comments:
Post a Comment