HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, November 5, 2017

NAIBU WAZIRI WA NISHATI, SUBIRA MGALU ATEMBELEA MIRADI YA UMEME CHAMAZI-DOVYA NA MBANDE WILAYANI TEMEKE

Naibu waziri wa Nishati, Mhe. Subira Mgalu, (kulia) akizungumza jambo mbele ya viongozi wa Tanesco mkoa wa Temeke na wa serikali ya Mtaa, alipotembelea miradi ya umeme huko Chamazi, Dovya, Mbagala jijini Dar es Salaam, leo Jumapili Novemba 5, 2017.

NA MWANDISHI WETU

NAIBU Waziri wa Nishati Mhe. Subira Mgalu leo Jumapili Novemba 5, 2017 amefanya ziara ya kutembelea miradi 7 ya umeme inayotekelezwa na Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), huko Chamazi-Dovya kwa Mzala 1-3, Mbande kwa Masister na Chamazi Vigoa, Mbagala jijini Dar es Salaam.

Katika ziara hiyo, Mhe. Waziri amefuatana na Kaimu Mkurugenzi, TANESCO, Mhandisi Dkt. Tito Mwinuka na viongozi wengine wa Shirika hilo.

Kwa mujibu wa Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Bi. Leila Muhaji, miradi hiyo saba ni pamoja na ule wa Chamazi Dovya ambao unajumuisha miradi mitatu, (3), Mbande kwa Masister, Miradio 4 na hivyo kufanya jumla ya miradi saba lengo likiwa ni kuwapatia umeme Wananchi wote wa Chamanzi Dovya ambao hawajapata umeme.
“Miradi hii imekamilika na na kila mradi tumefunga transfoma mbili (2).” Alisema Bi. Leila.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Dkt. Tito Mwinuka(wapili kushoto), Meneja Mwandamizi wa TANESCO Kanda ya Dar es Salaam na Pwani Mhandisi Mahende Mgaya, (wakwanza kushoto) wakimsikiliza Meneja wa TANESCO Mkoa wa Temeke, Mhandisi Jahulula, wakati akisoma taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo.
Naibu waziri Mgalu akiangalia ripoti ya utekelezaji wa miradi hiyo, iliyokuwa ikisomwa na Meneja wa TANESCO Mkoa wa Temeke, Mhandisi Jahulula Maendeleo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad