HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, November 28, 2017

MAWAZIRI WA UGANDA WAFANYA ZIARA NCHINI TANZANIA

 Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (kulia) akizungumza wakati wa mkutano na Ujumbe wa Mawaziri kutoka Uganda. Katikati ni Waziri wa Nchi- Madini, Lokeris Peter na Waziri wa Nchi- Mambo ya Ndani, Obiga Kania. 
 Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (kushoto) akizungumza wakati wa mkutano na Ujumbe wa Mawaziri kutoka Uganda (hawapo pichani). Katikati ni Kamishna wa Madini, Mhandisi Benjamin Mchwampaka na Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST), Profesa Abdulkarim Mruma.
 Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (mbele katikati) akizungumza wakati wa mkutano na Ujumbe wa Mawaziri kutoka Uganda (kushoto) na baadhi ya Watendaji wa Wizara na Taasisi zilizochini ya Wizara ya Madini (kulia).
 Mawaziri kutoka Uganda wakimsikiliza Waziri wa Madini nchini, Angellah Kairuki (hayupo pichani). Kutoka kulia ni Waziri wa Nchi- Madini, Lokeris Peter, Waziri wa Nchi- Mambo ya Ndani, Obiga Kania, Waziri wa Nchi- Mamlaka ya Mji Mkuu wa Kampala,  Namugwanya Bugembe na Waziri wa Nchi- Masuala ya Uchumi, Dkt. Kasirivu Atwooki.
 Kamishna wa Madini, Mhandisi Benjamin Mchwampaka akiwasilisha mada ya masuala mbalimbali ya Sekta ya Madini, nchini Tanzania.
Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (kulia) akimsikiliza Waziri wa Nchi- Mambo ya Ndani wa Uganda, Obiga Kania (kushoto). Katikati ni Waziri wa Nchi- Madini, Lokeris Peter. 

Waziri wa Madini, Angellah Kairuki amekutana na Mawaziri Wanne kutoka nchini Uganda ambao wamewasili nchini Tanzania kwa ajili ya ziara ya siku mbili ya kubadilishana uzoefu katika usimamizi wa Sekta ya Madini.
Mawaziri hao ni Waziri wa Nchi- Madini, Lokeris Peter, Waziri wa Nchi- Mambo ya Ndani, Obiga Kania, Waziri wa Nchi- Mamlaka ya Mji Mkuu wa Kampala,  Namugwanya Bugembe na Waziri wa Nchi- Masuala ya Uchumi, Dkt. Kasirivu Atwooki.
Waziri Kairuki amekutana na ujumbe huo Novemba 28, 2017 katika Ofisi za Wizara ya Madini jijini Dar es Salaam na kujadiliana masuala mbalimbali ya uendeshaji wa shughuli za Madini nchini ikiwemo suala la Sera, Sheria na Kanuni za Madini pamoja na masuala yanayohusu Wachimbaji Wadogo wa madini.
Majadiliano baina ya Wizara na Ujumbe huo vilevile yalihusisha uwasilishaji wa mada mbalimbali kutoka kwa Kamishna wa Madini, Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO).
Ujumbe huo utatembelea migodi mbalimbali ya Dhahabu inayomilikiwa na wazawa iliyoko mkoani Geita ili kujionea uendeshaji wa migodi hiyo na hivyo kupata uzoefu wa namna ya uendeshaji wake.
Aidha, ujumbe huo wa Mawaziri kutoka nchini Uganda, utatembelea nchi mbalimbali Barani Afrika ili kupata uzoefu wa usimamizi wa Sekta ya Madini hususan suala la Wachimbaji Wadogo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad