HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, November 9, 2017

JUMUIYA WAFANYABIAASHARA WA JAMHURI YA CONGO WAISHIO NCHINI WAMEIPONGEZA SERIKALI KWA KUONDOA VIKWANZO KATIKA BANDARI YA DAR ES SALAAM.


Rais Jumuiya ya Wafanyabishara wa Congo nchini, Mukendi kabobu akizungumza na waandishi wa habari juu ya hatua ya kuondolewa kwa vikwazo vya kibiashara katika bandari ya Dar es Salaam.


Jumuiya ya wafanyabiaashara wa jamhuri ya Congo waishio nchini wameeleza kuridhshwa na mazingira ya ufanyaji wa biashara nchini ukiligansha na ilivyokua awali ambapo ilikua na changamoto mbalimbali.

Wakizungumza na waandishi kwa kutatua changamoto walizozilalamikia ikiwemo Urasimu wa utoaji wa mazigo bandarini ,Wamesema hapo nyuma kulikuwa na urasimu ulisababisha idadi kubwa ya wafanyabiashara wanaotoka nchini Congo kukacha kutumia bandari ya Dar es salaam.

Rais wa Jumuiya ya Wafanyabishara wa Congo nchini, Mukendi kabobu, amesema wanaipongeza serikali ya Tanzania kupitia kwa Rais Dk.  John Pombe Magufuli kwa kuondoa vikwazo vya kibiashara katika uondoshaji wa mizigo katika bandari ya Dar es Salaam.

Amesema kuwa wafanyabiashara wa Congo kila wakiwa na mambo ambayo yamekuwa kikwazo kwao yamekuwa yakitatuliwa na kufanya biashara kuwa nyepesi katika kupitishia bandari ya Dar es Salaam.

Makamu wa Rais Jumuiya hiyo,John Kapeta amesema kuwa wa wafanyabiashara wanaotoka nchi ya Congo wanafanya biashara bila kikwazo kutokana na jitihada alizochukua Rais Dk. John Pombe Magufuli juu ya uboreshaji wa huduma katika bandari ya Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jumuiya ya Wafanyabishara wa Congo nchini, John Kapeta akizungumza na waandishi habari juu ya urahisi wa kupata huduma katika bandari ya Dar es Salaam pale wanapotaka kuotoa mizigo mkutano ulifanyika jijjini Dar es Salaam.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad