Baada
ya kuumia katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mtibwa mshambuliaji wa Yanga
Donald Ngoma na kushindwa kufanya mazoezi jana pamoja na kikosi kutokana na
maumivu ya misuli siku ya Jumamosi.
Ngoma
baada ya kuumia hakuweza kurejea tena uwanjani na nafasi yake kuchukuliwa na
Juma Mahadhi, siku ya jana hakufanya mazoezi pamoja na wachezaji
wenginena kupewa mapumziko na daktari wa timu Hussein Bavu.
Ngoma
alipewa saa 24 hadi 48 za uangalizi chini ya daktari wa Yanga ili kuona
maendeleo kabla ya kutoa majibu kama anaweza kurudi uwanjani mapema au
vinginevyo.
Dakatri
wa timu hiyo Bavu amesema kuwa baada ya masaa 24 hadi 48 ndipo wanaweza kutoa
majibu sahihi kwani kwa sasa wamempa mapumziko Ngoma ili aweze kurejea katika
hali ya kawaida na kuangalia maendeleo yake.
Kwa
sasa maendeleo ya Ngoma yanaendelea vizuri na anatembea vizuri ukilinganisha na
ilivyokuwa mwanzo, anaweza kufanya mazoezi binafsi ikiwa ni tiba ya jeraha lake
Yanga
inakabiliwa na mchezo wa raundi ya sita ya ligi kuu VPL dhidi ya Kagera Sugar
October 14, 2017 kwenye uwanja wa Kaitaba, mkoani Kagera.
No comments:
Post a Comment