HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, September 12, 2017

NE-MO AJA TENA KUACHIA NGOMA MPYA 'KIPOTABO" SEPT 19


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MSANII wa muziki wa kizazi kipya Shaban Mpute 'Ne-Mo' amesema amedhamiria kurudi katika familia ya muziki kivingine, huku akitarajia kuachia wimbo wake mpya unaitwa 'Kipotabo'Septemba 19 mwaka huu ambayo imetengenezwa katika studio za Combination Sound chini ya mtayarishaji Man Water na video kutengenezwa na Kwetu Studio.

Akizungumzia ujio wake  mpya Ne-Mo chini ya lebo ya 'Digital City Drimz' alisema kuwa amedhamiria kuirejesha RnB ya Bongo katika viwango na pia kuipeleka nje ya mipaka ya Tanzania, kwa sababu anahifahamu vizuri na  kwa sasa kuna wasanii kama Diamond Platnumz, Ali Kiba, Vanessa Mdee, Navy Kenzo na wengineo wameubeba muziki wa Bongofleva na kusaidia kuupenyeza kimataifa, naye ana matumaini makubwa ya kufika walipo wasanii hao.

Ne-mo ujio wake utakuwa wa aina yake na Watanzania hawatajutia kumsubiri Ne-Mo arudi kwa muda wote huo, kwamba ukimya wake umetokana na masomo ambapo aliamua kutulia amalizie masomi kisha aendelee na Harakati za Muziki na  alikuwa masomoni akiwa amesomea  masuala ya  'Mass Communication' na anaeleza kuwa sasa ametulia na amepata 'Mameneja ' ambao wanamsimamia na kumrejesha kwa kishindo katika muziki.

"Nimejipanga vuzri pamoja na mameneja wangu narudi kimuziki kikweli kweli, naomba mashabiki wa muziki Tanzania wanipokeekwa mara nyinyingine, nilitoka kidogo kwenda masomini lakini sasa nimerudi rasmi katika muziki"alisema Ne-mo.

Alisema kwa upande wa mtindo wa Rap na Hip Hop mwanzoni mwa miaka ya 2000 Profesa Jay alichangia kuuweka muziki wa Hip Hop mtaani na kukubalika na kila kundi la jamii., miaka michache iliyopita waliibukakina Child Benz na Nako 2 Nako ambao walisaidia kujenga misingi ya kuufanya muziki wa Hip Hop kukubalika kibiashara.

Alisema sasa hivi wasanii kama Weusi, Darasa, Billnas, Young Dee na kadhalika ambao wanauwekea vionjo muziki wa Rap kufanya kupenya zaidi na hata uanze kuimbwa na hata akina dada ambao zamani ilikuwa ni nandra kuwa na mapenzi na muziki wa Rap.

Meneja wa mwanamuziki huyo Habibu Anga 'Guru Picasso' alisema kuwa siku ya Jumatatu wataachia rasmi wimbo wa Kipotabo wa msanii huyo na amekuja kuitikisa zaidi Tanzania na Afrika Mashariki kama ilivyotokea  mwaka 2013 alipoachia wimbo uliokwenda kwa jina la "Number One" ambao alimshirikisha mkali mwenzake 'Ommy Dimpoz' wimbo ambao ulikuwa mkubwa na kugeuka kama 'wimbo wa Taifa' kama wasemavyo mtaani.

Baada ya mafanikio makubwa ya wimbo huu wa 'Number One' Ne-Mo hakuwahi kutoa kazi yake nyingine yoyote ile, zaidi ya nyimbo za kushikishwa ambazo ni 'Mrs Superstar' ya Young Killer, 'Tulikuwepo' ya Niki Mbishi, 'Sijutii' ya Msamiati na nyinginezo nyingi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad