Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kulia) akizungumza na Balozi wa Sweden Nchini, Katarina Rangnitt (kushoto) katika kikao chake kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Nishati na Madini zilizopo jijini Dar es Salaam tarehe 22 Septemba, 2017. Kikao hicho kilishirikisha wataalam kutoka Idara ya Nishati, Wizara ya Nishati na Madini, na Mamlaka ya Udhibiti wa Shughuli za Mkondo wa Juu wa Mafuta (PURA).
Sehemu ya wajumbe wa kikao hicho wakifuatilia maelekezo yaliyokuwa yanatolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (hayupo pichani).
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Shughuli za Mkondo wa Juu wa Mafuta (PURA), Chalers Sangweni (kulia) na mjiolojia kutoka mamlaka mamlaka hiyo, Simon Nkenyeli (kushoto) wakifuatilia majadiliano mbalimbali katika kikao hicho.
Mtaalam wa Masuala ya Nishati kutoka Ubalozi wa Sweden Nchini, Jorgen Eriksson (kushoto) akieleza jambo katika kikao hicho. Kulia ni Balozi wa Sweden Nchini, Katarina Rangnitt.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (katikati) na Balozi wa Sweden Nchini, Katarina Rangnitt ( wa nne kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kikao hicho.
No comments:
Post a Comment