HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, August 24, 2017

MKAZI WA LINDI ALAMBA KITITA CHA ZAIDI YA MIL 118/- M-BET

 Kaimu Mkurugenzi wa  Uendeshaji na Sheria wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini, James Mbalwe(kulia) na Afisa habari wa M-BET,David Malley(katikati)wakimsikiliza mshindi waM-BET aliyejishindia zaidi ya shilingi milioni  118/- Erick Matey,Ambaye ni mkazi wa mkoa wa Lindi,Wakati wa hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam ya kumkabidhi mshindi huyo hundi yake aliyojishindia  kupitia mchezo wa kubahatisha Supper 12 unaoendeshwa na M-bet.
  Kaimu Mkurugenzi wa  Uendeshaji na Sheria wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini, James Mbalwe(wapili kushoto) na Afisa habari wa M-BET,David Malley(kulia)wakimpongeza kwa kumpigia makofi mshindi wa zaidi ya shilingi milioni wa zaidi 118/- Erick Matey ambaye ni mkazi wa mkoa wa Lindi,Wakati wa hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam ya kumkabidhi mshindi huyo hundi yake aliyojishindia  kupitia mchezo wa kubahatisha Supper 12 unaoendeshwa na M-bet.
 Mshindi wa kitita cha zaidi ya shilingi milioni wa zaidi 118/- Erick Matey ambaye ni mkazi wa mkoa wa Lindi(kushoto)akikabidhiwa hundi yake na Afisa habari wa M-BET,David Malley(kulia)anaeshuhudia katikati ni Kaimu Mkurugenzi wa  Uendeshaji na Sheria wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini, James Mbalwe.
 Mshindi wa kitita cha zaidi ya shilingi milioni wa zaidi 118/- Erick Matey ambaye ni mkazi wa mkoa wa Lindi(kushoto)akiwaonesha hundi yake waandishi wa habari(hawapo pichani) Wakati wa hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam ya kumkabidhi mshindi hiyo aliyojishindia  kupitia mchezo wa kubahatisha Supper 12 unaoendeshwa na M-bet,Wapili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa  Uendeshaji na Sheria wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini, James Mbalwe na Afisa habari wa M-BET,David Malley.
 Mshindi wa kitita cha zaidi ya shilingi milioni wa zaidi 118/- Erick Matey ambaye ni mkazi wa mkoa wa Lindi,akiwa ameshikilia hundi yake mara baada ya kukabidhiwa rasmi leo wakati wa hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam ya kumkabidhi mshindi hiyo aliyojishindia  kupitia mchezo wa kubahatisha Supper 12 unaoendeshwa na M-bet.

Na Mwandishi wetu
MKAZI wa mkoa wa Lindi Mjini, Erick Matey mwenye umri wa miaka 26 ameibuka mshindi baada ya kubashiri vyema matokeo ya mechi kupitia Kampuni ya m-Bet na kujishindia zaidi ya Shilingi Milioni 118/-.

Matey amekabidhiwa fedha zake leo katika hafla  fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana

Kwa upande wake, Afisa habari wa  M-Bet, David Malley alisema kuwa Matey alifanikiwa kuzoa kitita hicho baada ya kufanikiwa kutabiri matokeo ya mechi 12 za ligi ya Ulaya kwa mtindo wa kucheza kawaida yaani super 12.

“Tunafarijika kumkabidhi Matey kitita hicho cha aidi ya Sh milioni 118/- akiwa ndiye mshindi wa m-Bet ambapo atapata Sh milioni 97/- baada ya makato ya kodi,” alisema Malley.

Aliwataka watanzania kuchangamkia kutumia mtandao wa intaneti kuonyesha ushabiki halisi wa soka akisema kuwa Perfect 12 ni mchezo wa ziada unaoruhusu kutabiri mechi 12 kwa Tsh 1,000 tu ambapo ukipatia zote  unaondoka na kitita chako mchana kweupe.

Naye Mshindi huyo, Erick Matey amewashauri watanzania wote wenye umri unaoruhusiwa kisheria kujitokeza kubashiri matokeo ya mechi mbalimbali kupitia Kampuni ya m-Bet .

"Nashukuru sana m-Bet kwa kuniwezesha kujikwamua kimaisha, nitatumia fedha hizi kutimiza ndoto yangu ya kununua kiwanja na kuanza ujenzi", alisema Matey

Kuhusu m-Bet, ni Kampuni iliyosajiliwa chini ya Sheria za Tanzania na kupewa leseni na Bodi ya Michezo ya kubahatisha tanzania kwa lengo la kufanya upatikanaji rahisi na mwingiliano wa huduma ya mchezo wa kubahatisha (Sim Betting) nchi nzima

“Kushiriki, ingia www.m-bet.co.tz, chagua kucheza kawaida au Perfect 12 ambapo kwa Shilingi 1000, unachagua matokeo 12. Ukipata yote sawa, unanyakua kikapu cha m-Bet,” alisema Malley.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad