HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, August 24, 2017

MSD NA WIZARA YA AFYA WASAINI MKATABA NA KAMPUNI YA ZIPLINE KWAAJILI YA KUSAMBAZA DAWA.

WIZARA  ya afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto na Bohari ya Dawa Tanzania(MSD) wamesaini mkataba wa makubaliano na kampuni ya Zipline jijini Dar es Salaam leo kwaajili ya kuanza kujenga vituo vya kurushia Drone za kusafirishia dawa kataka maeneo mbalimbali hapa nchini wakianzia na Mkoa wa Dodoma na Mwanza.

 akizungumza wakati wa kusaini na kubadilishana mikataba ya makubaliano, Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya amesema kuwa  mradi huo umekuja wakati muafaka kutokana na ukuaji wa Teknolojia Bohari ya Dawa Tazania itapata urahisi wa kusambaza zawa katika vituo mbalimbali vya Afya.

Amesema kuwa  kwa kuanza mradi huo utaanza kwa kusambaza dawa ambazo zinaubaridi kama Damu katika vituo 200 vya mkoa wa Dodoma ambapo baada ya hapo watandelea na mikoa ya Kanda ya ziwa na baadae nchi nzima.

 Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Zipline, Keller Rinaudo,amesema kuwa Mradi huo umefanikiwa kwa kiasi kikubwa nchini Rwanda na hapa nchini utaenda vyema zaidi pia amesema kuwa utatoa ajira nyingi kwa vijana wa kitanzania ambao watakuwa na mawazo mazuri ya ubunifu kwaajili ya kuendeleza kuenea mradi huo hapa nchini.


Mkurugenzi Mkuu Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu wakibadilishana mkataba wa makubaliano na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Zipline, Keller Rinaudo wakibadilishana kwaajili ya kuanza kujenga vituo vya kurushia drone zitakazo kuwa zikisafirisha dawa katika maeneo mbalimbali ya nchi. Ktikati ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya akisuhudia wanavyobadilishana mikataba hiyo jijini Dar es Salaam leo.
  
Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya akizungumza wakati wa kusaini Mkataba kati ya wizara ya Afya, Bohari ya Dawa Taznania(MSD) na Kampuni ya Zipline kwaajili ya kuanza kufanya utafiti wa maeneo yatakayojengwa kwaajili ya sehemu ambapo Kampuni ya Zipline itakuwa ikirushia vifaa maalum ambazo ni Drone zitatumika kusambaza dawa katika mikoa maeneo ambayo ni ngumu kufikika kwa urahisi kutokana na umbali wake.
 Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Zipline, Keller Rinaudo, akizungumza wakati wa kusaini Mkataba wa Makubaliano kuanza kujenga vituo kwaajili ya kurushia Drone ambazo zitakuwa zikisafirisa dawa kwenye maeneo ambayo hayafikiki kwa urahisi ikiwa mradi huo utaanza katika mikoa ya Dodoma na Mwanza. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu na Kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Dkt. Mpoki Ulisubisya, Mkurugenzi Mkuu Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Bwanakunu na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Zipline, Keller Rinaudo wakisaini mkataba wa kuanza kujenga vituo vya kurushia Drone zitakazo kuwa zikisafirisha dawa kwenye maeneo ambayo hayafikiki kwa urahisi. Kulia ni Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Bakari Kambi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad