HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, August 30, 2017

KESI YA RAIS WA SIMBA NA MAKAMU WAKE YAENDELEA KUPIGWA KALENDA

Kwa mara nyingine tena upelelezi dhidi kesi ya utakatishaji fedha na kugushi inayomkabili Rais wa  Klabu ya Simba, Evans Aveva na Makamu wake Godfrey Nyange Kaburu umedaiwa kuwa bado kukamilika na kwamba kuna nyaraka mbalimbali zimepelekwa kwa mtaalamu wa maandishi.

Wakili wa serikali, Eatazia Wilson amedai hayo leo mbele ya Hakimu Mkazi Victoria Nongwa, pindi kesi hiyo imekuja kwaajili ya kutajwa na kudai bado wanasubiri ripoti ya polisi.

Kufuatia taarifa hiyo, Hakimu Nongwa aliutaka upande wa jamuhuri kujitahidi kuharakisha upelelezi kwasababu washtakiwa wapo ndani na kwamba
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 8 mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.

Aveva na Kaburu  wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha fedha USD 300,000.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad