HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, August 31, 2017

KESI MASOGANGE YAPIGWA KALENDA.

Video Queen, Agnes Gerlda, maarufu kama Masogange (Kulia), akiwa na mpambe wake wakitoka katika viunga vya mahakama ya hakimu mkazi Kisutu   ambapo amepatikana na kesi ya kujibu katika tuhuma za matumizi ya dawa za kulevya zinazomkabili mahakamani hapo uamuzi uliotolewa na Hakimu Wilbard Mashauri.

Akisoma uamuzi huo baada ya shahidi Wa mwisho Wa upande wa mashtaka kumaliza kutoa ushahidi wake, hakimu Mashauri amesema, baada ya kusikiliza ushahidi wa upande wa mashtaka ameridhika kuwa mshtakiwa ana kesi ya kujibu na kumtaka ajiandae kujitetea.

Mshtakiwa Msogange amedai kuwa atajitetea kwa kiapo na pia atakuwa na mashahidi watatu watakaofika mahakamani hapo kumtetea.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 12, mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad