HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, July 26, 2017

SUKOS yakabidhi Vifaa vya Zimamoto Hospitali ya Muhimbili Leo

Taasisi ya Maafa, Majanga na Uokoaji -SUKOS, leo ameikabidhi Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) vifaa vya zimamoto ili kusaidia uokozi mara yanapotokea majanga ya moto.

Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Suleiman Kova amesema wameamua kutoa msaada huo katika hospitali hiyo kwa kuwa imekuwa ikitoa huduma nzuri za afya.

“Tulifanya utafiti tukavutiwa na huduma nzuri zinazotolewa Muhimbili hivyo tumeanza na Muhimbili na baadaye tutaenda kutoa msaada kwenye taasisi nyingine. Kama mnavyojua tunafanya kazi ya kijitolea,” amesema Kova.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Profesa Lawrence Museru ameshukuru Muhimbili kupatiwa msaada huo na kwamba vimetolewa wakati muhafaka.

Mkurugenzi wa Ufundi, Gaudence Aksante amesema vifaa hivyo vitatunzwa ili viweze kutoa huduma iliyokusudiwa.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Maafa, Majanga na Uokoaji -SUKOS, Suleiman Kova (kulia) akimkabidhi vifaa vya zima moto Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru kwa ajili ya kutoa huduma ya uokoaji endapo itatokea majanga ya moto katika maeneo ya kazi au majumbani. Kulia ni Mkurugenzi wa Ufundi, Gaudence Aksante.
Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Profesa Lawrence Museru akishukuru baada ya kupokea msaada huo Leo. Kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Suleiman Kova na Mkurugenzi wa Ufundi, Gaudence Aksante akifuatilia tukio hilo.
Meneja wa Masoko na Mauzo wa Kampuni ya Astrade Tanzania, Abdallah Massawe akielezea matumizi ya kifaa maalumu cha kutoa taarifa mara gesi inapokuwa ikivuja kwenye mtungi. Kifaa hicho kinasaidia watumiaji wa gesi kuchukua taadhari mara gesi inapoanza kuvuja.
Mmoja wa wafanyakazi wa Taasisi ya Maafa, Majanga na Uokoaji –SUKOS, Ramadhani KHamisi akionyesha jinsi ya kuzima moto baada ya kutokea mlipuko sehemu za kazi au majumbani.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad