HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, July 14, 2017

DISMAS TEN RASMI NI MKUU WA KITENGO CHA HABARI WA YANGA SC


Klabu ya Yanga leo imemtangaza rasmi aliyekuwa afisa habari wa klabu ya soka ya Mbeya City Bwana Dismas Ten kama afisa habari wao baada ya kuingia nae mkataba leo. 

Dismas anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa afisa habari wa klabu hiyo Jerry Murro ambaye mwaka jana 09 Julai 2016 alifungiwa na Shirikisho la soka nchini kujihusisha na soka.

Nafasi hiyo ilikuwa ikikaimiwa na Godlisten Anderson Chicharito kama kaimu afisa habari ambaye sasa ataendelea na nafasi hiyo chini ya Dismas Ten. 

"Tumeamua kuleta mapinduzi kwenye utoaji habari kwenye klabu yetu na naamini kwa muunganiko huu wa Dismas na Chicharito klabu yetu itafanikiwa sana kupitia kitengo iki cha Habari na mawasiliano kama vilabu vingine vikubwa duniani."-Boniface Mkwasa Katibu Mkuu Yanga SC.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad