Taasisi
ya kuzuia na kupambana Rushwa nchini (TAKUKURU),imewafikisha Mahakama
ya Hakimu Mkazi Kisutu watu wawili James Rugemalira (Pichani kushoto) na
Harbinder Seth Sigh (Pichani kulia) kwa tuhuma ya kesi ya Uhujumu
Uchumi.
Akizungumza
mapema leo mchana jijini Dar Es Salaam,Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya
Kupambana na Kuzuia Rushwa nchini (TAKUKURU), Valentino Mlowola amesema
kuwa Mmiliki wa VIP Engineering and Marketing, James Rugemalila na
Mmiliki wa Kampuni ya IPTL, Harbinder Seth Sigh wamefikishwa mahakama ya
Kisutu leo mchana kwa kosa la kuhujumu uchumi pamoja na makoasa mengine
yanayofanana na hayo.
Mlowola
amesema kuwa watuhumiwa hao wameshafikishwa mahakamani kwa kosa la
kuhujumu uchumi pamoja na makosa yanayofanana na hayo,akaongeza kusema
kuwa TAKUKURU wamechunguza shauri hilo kwa muda mrefu na sasa imefika
wakati kuwapeleka mahakamani watuhumiwa hao kujibu mashtaka yao.
Mlowola
ametoa Wito kwa wananchi kutambua kuwa serikali ina nia njema na dhati
kabisa ya kuwapa Maisha bora Watanzania,hivyo hakuna budi wale wote
wanaotuhumiwa kwa makosa mbali mbali watafikishwa mbele ya vyombo vya
sheria.
Kabla
ya vigogo hawa wawili kufikishwa mahakamani leo,
baadhi ya watumishi wa TANESCO tayari walishtakiwa kufuatia tuhuma za
kupokea fedha kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya VIP Engeneering and
Marketing ambaye pia alikuwa Mkurugenzi wa kampuni ya kufua
umeme ya Independent Power Tanzania Ltd (IPTL), James Rugemalira.
Mmiliki wa VIP Engineering and Marketing, James Rugemalila na Mmiliki wa Kampuni ya IPTL, Harbinder Seth Sigh wakiwa wamechuchumaa kabla ya kupelekwa kwenye chumba cha mahakama kwa ajili ya kusomewa mashitaka yao,likiwemo la Uhujumu uchumi
Mmiliki wa VIP Engineering and Marketing, James Rugemalila na Mmiliki wa Kampuni ya IPTL, Harbinder Seth Sigh wakiwa ndani ya chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu tayari kwa kusomewa mashitaka yao,likiwemo la Uhujumu uchumi.
No comments:
Post a Comment