HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, June 19, 2017

ASKARI WA USALAMA BARABARANI WAFANYA UKAGUZI MABASI WA KITUO KIKUU CHA MABASI UBUNGO

Mkaguzi wa Polisi katika Kituo cha cha Mabasi Ubungo, Inspekta Ibrahim Samwix katika uvungu wa basi akikagua basi katika kikuu cha mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani.
Mkaguzi wa Polisi katika Kituo cha cha Mabasi Ubungo, Inspekta Ibrahim Samwix akikagua moja ya basi katika kituo hicho kikuu cha mabasi ya mikoani na nje ya nchi leo jijini Dar es Salaam ikiwa ni utaratibu wa ukaguzi kabla ya mabasi hayo hajaanza safari.
Askari wa Kikosi cha usalama barabarani kituo cha Ubungo, Nuru Mvungi akikagua mikanda katika basi la Kampuni ya Mlola inayofanya safari zake Dar es Salaam na Tanga leo jijini Dar es Salaam.
Askari wa Kikosi cha usalama barabarani kituo cha Ubungo, akionesha basi la Cheeter linalofanya safari zake Dar es Salaam na Dodoma likiwa limetolewa namba za usajili kutoka na ubovu na basi hilo linatakiwa kufanya safari baada kufanyiwa marekebisho leo jijini Dar es Salaam.

Askari wa Usalama barabarani wakiwa katika maandalizi ya ukaguzi wa mabasi ya mikoani na nchi jirani leo jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya mabasi yakiwa katika kituo kikuu cha Ubungo leo jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad