HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, June 6, 2017

OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU YAENDESHA MAFUNZO KWA AJILI YA UTAFITI WA MAPATO NA MATUMIZI YA KAYA BINAFSI TANZANIA BARA WA MWAKA 2017/18

 Mkufunzi anayesimamia mafunzo ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi Tanzania Bara wa Mwaka 2017/18 (2017/18 HBS) Sergiy Redyakin akimwelekeza mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) namna ya kujaza dodoso litakalotumika katika utafiti huo unaotarajia kufanyika nchini kuanzia mwezi Agosti, 2017.
 Baadhi ya Watakwimu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wakifuatilia kwa makini mafunzo yanayotolewa na mkufunzi anayesimamia mafunzo hayo Sergiy Redyakin (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi Tanzania Bara wa Mwaka 2017/18 yaliyofanyika hivi karibuni katika makao makuu ya NBS Dar es Salaam.
 Baadhi ya watakwimu kutoka NBS wakijifunza namna ya kujaza madodoso kwa njia ya kieletroniki wakati wa mafunzo ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi Tanzania Bara wa Mwaka 2017/18 unaotarajia kufanyika nchini kuanzia mwezi Agosti, 2017.
Mtakwimu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Hellen Mtove (wa kwanza kulia) akimhoji mmoja wa wanakaya wakati wa majaribio ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi Tanzania Bara wa Mwaka 2017/18 unaotarajia kufanyika nchini kuanzia mwezi Agosti, 2017.

(PICHA NA EMMANUEL GHULA)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad