HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, April 20, 2017

NEEMA YANGA YAANZA KUNUKIA, SPORTSPESA KUMWAGA MANOTI


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii



IKIWA katika hali ya kuyumba kiuchumi na kushindwa kuwalipa wachezaji wao mishahara kwa wakati, neema imeanza kuwaangukia baada ya kampuni ya SportsPesa ya Kenya kutaka kuwamwagia fedha iwapo mkataba wao utafanikiwa.

Yanga itakuwa ni ya tatu kwa timu za Afrika Mashariki kuingia mkataba wa fedha nyingi iwapo watakapofanikiwa kumalizana kumalizana na Kampuni ya SportsPesa ya Kenya.

Iwapo mkataba huo utafanikiwa, Yanga na kampuni hiyo ya SportsPesa watasaini mkataba wenye thamani ya bilion 4.5 ambapo utakuwa ni wa miaka mitano ambapo kwa mwaka utakuwa na thamani ya Sh milioni 900.

Uongozi wa Yanga leo unatarajiwa kutakutana na wawakilishi wa kampuni hiyo, ambapo wakikubaliana wataingia mkataba huo wa miaka mitano ambao kila mwaka utakuwa na nyongeza ya asilimia sita ya fedha.

Awali, SportsPesa walileta mapendekezo katika klabu ya Yanga kuhusiana na mkataba huo lakini ulikatiliwa kutokana na mkataba huo kutokukidhi vigezo nan kuwa na maslahi na wakawapelekea mapendekezo yao na namna gani wanataka mkataba huo uweje.

"\Leo wawakilishi wa SportPesa watakutana na uongozi wa Yanga ili kumalizana nao juu ya mkataba wanaotaka kuingia na hiyo ni kutokana na kufika makubaliano ya kimkataba," kiisema chanzo kutoka kamati ya utendaji ndani ya klabu hiyo.

Alipotafutwa Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Mkwasa, ambaye alisema wapo kwenye hatua za mwisho za kuingia mkataba na SportsPesa.

"Napenda nizungumze kitu kilichokua tayari au kimekamilika hatua ya kuingia mkataba na SportsPesa bado, ila tutakutana nao kwa mazungumzo ya mwisho ambayo yatatoa jibu kama watatudhamini au la.

"Tunazungumza na SportsPesa kwa kuwa hawa wamekuja moja kwa moja kwetu tofauti na kampuni nyingine ambazo zinataka kutudhamini, lakini ipo kampuni tuliyoipa jukumu la kufanya mazungumzo nao nasi kutuletea taarifa ya kila kinachoendelea." alisema Mkwasa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad