HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, April 20, 2017

Onyesho la Harusi Trade Fair kufanyika Mei 12-13

Maonesho ya tisa ya Harusi Trade Fair yanatarajiwa kufanyika Mei 12 hadi 13 mwaka huu kwenye hoteli ya Golden Tulip Oyststerbay Jiji Dar es salaam ili kuwapatia maharusi uwanja wa kuchagua mahitaji yao yote kwa ukamilifu siku ya harusi yao.

Akizungumza na Waandishi wa habari, Meneja Biashara Hamis Omary amesema maonesho hayo ni ya kipekee kwa Afrika mashariki na hufanyika mara moja kwa kila mwaka.

"Tunawatangazia jamii kwa ujumla watarajie maonesho yakuvutia kuburudisha pamoja na nyakati rahisi kwa bwana Harusi na bibi harusi kuandaa vitu vyao vya harusi, vilevile kutakuwa na mitindo mipya mingi kutoka kwa wauzaji bora katika sekta ya harusi kila maonesho yanavyoendelea kukua kutoka hatua moja na kwenda hatua nyingine ndivyo ubora unavyoendelea kuongezeka" amesema
Meneja Masoko wa Kampuni ya 361 Degrees, Hamis Omar(kushoto) akizungumza na waandishi wa habari akizungumza kuhusu maonesho ya tisa ya Harusi Trade Fair yanatarajiwa kufanyika Mei 12 hadi 13 mwaka huu kwenye hoteli ya Golden Tulip Oyststerbay Jiji Dar es salaam.
Kaimu Meneja wa Hoteli ya Golden Tulip, Adele Johnson(kushoto)  akizungumzia na waandishi wa habari leo kuhusu jinsi walivyodhamini maonesho ya tisa ya Harusi Trade Fair yanayotarajiwa kufanyika Mei 12 hadi 13.
Mratibu wa matukio wa Kampuni ya 361 Degrees, Naomi Godwin akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio waliyoyapata kwenye maonesho yaliyopita.
Mmoja wa waandishi wa habari akiuliza swali kwenye mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Maelezo jijini Dar leo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad